Showing posts with label MATUKIO. Show all posts
Showing posts with label MATUKIO. Show all posts

MMMHHHH LAANA HII...!! MAMA MTU MZIMA ANASWA AKINYONYESHA MBUZI BADALA YA MTOTO WAKE..JIONEE HAPA

 
 Vituko vya wanawake duniani, mwanamke akitumia matiti yake kumpa mazia mbuzi, picha za ajabu.

KWELI POMBE SIYO CHAI..!! NJEMBA WALEWA CHAKALI NA KULALA MCHANA KWEUPEE..TAZAMA PICHA HAPA

Hawa jamaaa walikutwa mchana kweupe wamezima kwa kunywa Pombe nyingi na kuzidiwa..Muda huo wa mchana walitakiwa wawe kazini wakijenga Taifa lakini wao mi mitungi kwenda mbele.

HIVI MAVAZI KAMA HAYA SEHEMU ZA KAZINI YANAASHIRIA NINI....??

 
HAPA INAKUAJE,MWANAFUNZI ATAELEWA KWELI JAMANI?!!
Siku zote ukijiheshimu utaheshimiwa, kujiheshimu huko ni pamoja na mavazi tunayovaa jamani.....sasa imagine mwalimu anavaa mavazi kama haya ...wanafunzi wataelewa kweli?? ukizingatia kizazi hiki cha google...Tubadilike jamani !!

MKE: NILIOLEWA ILI NIAMBUKIZWE UKIMWI...!! SOMA MKASA HUU WA KUSIKITISHA

UKISIKIA simulizi ya Hafsa Ramadhani (19) itakutia simanzi, itakutesa moyo na kukutoa machozi, huwezi kuamini aliingia kwenye ndoa bila kujua kuwa alikuwa akienda kukutana na ugonjwa wa ukimwi, Risasi Mchanganyiko linakufunulia.
Hafsa Ramadhani.
Habari kutoka chanzo chetu cha kuaminika zinasema, binti huyo alifanyiwa mipango ya ndoa bila yeye na mumewe huyo kupima kwanza maambukizi ya ugonjwa huo, ingawa tahadhari hiyo ilitolewa mapema kwa kuwa muoaji alikuwa akijulikana kuwa aliishi na ugonjwa huo kwa muda mrefu.
ILIKUWAJE?
“Huyo binti alitokea Bukoba, akaja hapa Dar es Salaam kutafuta kazi. Akaanza kufanya kazi za ndani, akiwa mdogo kabisa. Alihangaika kwenye nyumba mbalimbali lakini baadaye akafikia kwenye kituo cha watoto yatima (kwa sasa tunahifadhi jina), kipo Charambe ambapo alianza kuishi hapo,” kilipasha chanzo chetu kwa sharti la kutotajwa jina lake gazetini.
“Alipofikisha umri wa miaka 15 tu, wale watu wa pale kituoni wakamuozesha kwa jamaa mmoja (jina tunalo) ambaye kwa sasa ni marehemu. Huyo jamaa alikuwa akiishi na VVU na mbaya zaidi, hao watu wa hapo kituoni, walishauriwa kuhusu jambo hilo wakapuuza, ndiyo maana wengi wanaamini walimfanyia makusudi,” kilieleza chanzo hicho ambacho kimedai kipo karibu na binti huyo.
HUYU HAPA HAFSA
Timu ya gazeti hili kwa msaada wa chanzo chetu, ilifanikiwa kukutana na Hafsa ambaye kwa mwonekano ni binti mdogo na mpole kiasili, akazungumza mengi yanayomsibu katika maisha yake.
“Sikujua kama maisha yangu yangeishia hivi. Sikutegemea kama ningeteseka kiasi hiki. Kwanza mimi sijawahi kuwaona wazazi wangu. Niliambiwa tu walikufa tangu nikiwa mdogo, kwa hiyo nilikulia kwa wazazi wa kufikia huko Bukoba,” anaanza kusimulia Hafsa.
Akaendelea: “Baada ya kuolewa, maisha yalikuwa ya shida sana. Nilichukuliwa hapa Dar na kwenda kuishi na huyo mume wangu Arusha baada ya kufunga naye ndoa. Alikuwa haniachii fedha ya matumizi wakati mwingine lakini hali yake ya kuugua kila mara iliniogopesha ingawa sikuwahi kufikiria kabisa suala la ukimwi.
“Nilibahatika kupata mtoto na huyo bwana na hapo ukawa mwanzo wa mimi kuanza kuugua mfululizo. Nikiwa bado naumwa, mume wangu alifariki dunia. Basi, maisha yangu yakazidi kuwa magumu maana sikuwa na msaada wowote.”
DOKTA AMWAMBIA UKWELI
“Nikiwa nakwenda kliniki huku afya yangu ikiwa si ya kuridhisha, daktari mmoja alinishauri nifanyiwe vipimo. Ilibidi nishauriwe sana kabla ya kupimwa na kwa bahati mbaya nikagundulika kuwa nina ukimwi. Hata mwanangu pia ameathirika.
“Najua walinificha kwa muda mrefu kutokana na umri wangu, maana sasa nina miaka 19 na mwanangu mitatu, kwa hiyo wakati najifungua nilikuwa na 16 tu. Naiona dunia chungu kwa kweli.”
MAISHA MAGUMU ARUSHA, ARUDI DAR
“Kutokana na maisha ya mateso ya ndugu wa mume wangu kule Arusha, nilijikusanya nikapata nauli, nikaamua kutoroka na kurudi zangu Dar. Sikuwa na mahali pengine pa kwenda zaidi ya kurudi kituoni nilipokuwa nalelewa.”
ANYANG’ANYWA MWANAYE
“Mwanangu ndiye alikuwa faraja yangu pekee lakini wakwe zangu walikuja kuninyang’anya mtoto wakisema eti sina uwezo wa kumlea. Kwa kuwa ni damu yao, sikuwa na jinsi ikabidi nikubali tu. Sasa hivi anaishi nao huko Temeke.
“Nashukuru Mungu, nilipata msamaria (aliomba asitajwe jina lake) ambaye aliguswa na ugumu wa maisha yangu, akanikaribisha nyumbani kwake. Naishi naye Mbagala – Zakheem (Dar), lakini nina ugumu wa maisha. Kama unavyojua, siwezi kumtegemea yeye kwa kila kitu.”
ANAHITAJI MSAADA WAKO
Kama umeguswa na kisa cha Hafsa na ungependa kumsaidia kwa hali na mali, unaweza kufanya hivyo kwa kutumia namba 0783 855453 au 0713522779.

Aibu! Mke wa mtu anaswa wizi wa vitenge….!!

ANGEL Zambi ambaye ni mke wa mtu, mkazi wa Kitongoji cha Ipogolo mjini Iringa amenaswa akiiba vitenge na kanga kwenye duka moja, Risasi Mchanganyiko linakupa ‘ei tu zedi’.
Tukio hilo la aibu lilijiri Jumatatu iliyopita saa 5:10 asubuhi kwenye Mtaa wa Uhindini mjini Iringa jirani kabisa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kanisa Kuu.

Wakizungumzia tukio hilo, baadhi ya mashuhuda waliliambia gazeti hili kwamba, siku ya tukio, mwanamke huyo akiwa na wenzake watano walifika katika duka hilo la Elizabeth Mlowe kama wateja wa jumla wa nguo.

“Walimkuta binti muuzaji,  wakaanza kumsumbua kwa kuagiza nguo bila mpangilio, yule anaagiza aina ile  huku mwingine akiomba kusogezewa vitenge na kanga. Hali hiyo ilimchanganya muuzaji na kujikuta akiibiwa kirahisi na Angel,” alisema shuhuda mmoja.
vite

Akihojiwa na paparazi wetu, mwanamke huyo mwenyeji wa Mbeya aliyeolewa Iringa alisema kuwa alijiunga na mtandao wa wizi kwa kuzunguka madukani siku mbili zilizopita (Jumamosi).

Alisema kuwa mtandao huo unajulikana kwa jina la Zubaa Tutajirike (Zutu), upo Ipogolo kwa sasa lakini ulianzishwa jijini Mbeya ila baada ya kugundulika mbinu yao walihamia Iringa na kuendelea na wizi huo.
“Kwa kweli najuta sana,   ni mara yangu ya kwanza kuingia katika kazi hii hapa Iringa, wenzangu ambao wamenikimbia wao ni wenyeji. Mume wangu alinikataza kutembea nao, ila leo nimemtoroka,” alisema kisha kupelekwa polisi mjini hapa.



HURUMA: HAYA NDO MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA...TAZAMA HIZI PICHA DAH INASIKITISHA SANA...!!



Madereva wa malori zaidi ya mia tatu wamegoma kuendelea na safari katika barabara kuu itokayo Dodoma hadi Mwanza baada ya dereva mwezao aliyekuwa akiendesha lori kuvamiwa na majambazi katika eneo la kisaki manispaa ya Singida. 
 
Wakiongea na ITV /Radio one madereva ambao wamekutwa katika eneo hilo wameomba  jeshi la polisi kufanya doria mara kwa mara eneo hilo kwani kumekuwa na matuki  yanayo jirudia ya utekeji wa magari  kwa kuweka mawe makubwa barabarani na kuwajeruhi madereva jambo ambalo lina tishia amani kwa watumiaji wa barabara.
 
Madereva wa malori baada ya kufunga barabara naibu waziri wa Afrika mashariki Dr. Abdulla Abdulla alikumbwa na adha hiyo na kusema ni haki ya kikatiba kwa madereva kugoma kwa kudai haki zao, kutokana na hali hiyo amewahaidi madereva kupeleka kilio chao katika mamlaka husika ili kuweza kutatua tatizo lao na kukomesha vitendo vya uvamizi wa magari katika eneo hilo .
 
Kwa upande wake kamanda wa jeshi la polisi mkoani Singida  SACP Geofrey Kamwela amesema madereva waliamua kusimama barabarani bila sababu yeyote kwa muda wa zaidi ya masaa matatu na kusababisha foleni kubwa ambapo kwamujibu wa sheria za usalama barabarani walikuwa wamefanya kosa ,lakini baada ya viongozi kufika na kuwasikiliza waliamua kuendelea na safari.
 
Naye dereva wa lori bwana Agustino Mbawala aliye tekwa, akiwa amelazwa katika hospitali ya mkoa wa Singida akiongea kwa shida huku akiwa na maumivu makali amesema aliona mawe makubwa barabarani na kuamua kusimama na kukimbia lakini wali mvamia na kumpiga hatimaye  kumpora fedha na simu. 

>>ITV

HURUMA: HAYA NDO MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA...TAZAMA HIZI PICHA DAH INASIKITISHA SANA...!!















HII NI LAANA NA KUKOSA MAADILI...!! TAZAMA PICHA ALIYOPIGA HUYU DADA NA KUIWEKA MTANDAONI...

Hivi msichana unapopiga picha kama hii na kuiweka mtandaoni, unakuwa unafikiria nini...?? Mbadilike jamani wadada mnatuhaibisha sana..
  Bongonews ina laani vikali tabia hii iliyokithiri hapa nchini..

DEREVA BODABODA ACHEZEA KICHAPO TOKA KWA TRAFIKI JIONEE HAPA.

Dereva bodaboda (hakutambulika jina lake) baada ya kupokea kichapo cha askari wa usalama barabarani (nae hakutambulika jina)eneo la Vingunguti

                  ...akionesha uso wa hudhuni baada ya kichapo. 
Askari wa usalama barabaranui (hayupo pichani) anadaiwa kumjeruhi dereva bodaboda eneo la vingunguti jijini dar. Chanzo chetu cha habari kimeeleza kuwa, tukio hilo limetokea leo majira ya mchana wakati dereva huyo alipokutana na askari akiwa amebeba abilia wawili maarufu kama"mshikaki". baada ya askri huyo kutaka kupata maelezo ya kina kutoka kwa dereva huyo, ndipo ikatokea hali ya kutyoelewana ndipo askari huyo huyo aliamua kumzaba kibao na kumjeruhi kama picha zinavyoonesha hapo juu.
(PICHA NA: HARUNI SANCHAWA/ GPL)

Nesi Feki Anaswa Akiiba Kichanga Hospitalini… Apewa Kichapo na Kutembezwa Mtupu Barabarani

Nesi Feki

Nesi Feki Anaswa

Aibu Kubwa ya Kusikitisha, Kilichomkuta Dada Huyu Ama kwa hakika hawezi Kusahau Maishani Mwake . Nesi Feki  Ambaye Alinaswa Akiiba Mtoto Hospitalini Huko Nchini Ghana.
Tukio Hilo Lilitokea Wakati Dada huyo Alipoamua Kuvalia Sare za Hospitali kama Nesi na Kuamua Kuingia Wodi Ambayo Watoto Waliotoka Kuzaliwa Huhifadhiwa Kwa Muda kabla ya Kukabidhiwa kwa Mama zao.
Nesi Feki
Nesi Feki Anaswa Akitembezwa Mtupu
Baada ya Kufaulu Mtihani huo na Kuweza Kujipenyeza hadi kwenye Wodi Hiyo , Nesi Feki  Huyo Alimchukua Mmoja Kati ya Watoto Aliyeonekana Kuvtiwa nae na Kumficha Kwenye Begi Lake Akioekana kama Vile Amebeba Nguo.

Balaa Lamkuta

Balaa Lilimkuta Dada Huyo Kipindi Ambacho Alikuwa Akijaribu Kutoka Nje ya Hospitali Hiyo na Kwa Bahati Mbaya Mtoto Aliyekuwa Amemficha Ndani ya Begi Lake Akaanza Kulia Kwa Nguvu.

Mshangao

Walinzi wa Hospitali Ilibidi Kumzuia Kwa Muda Dada Huyo (Nesi Feki) Ili Kuweza Kumkagua na Kuona ni Kitu Gani Kilichopo Ndani ya Begi Alililokuwa Amelishikilia. Ndipo Kwa Mshangao Mkubwa Walinzi Walipomwona Mtoto huyo Mchanga Akiwa Ndani ya Begi Huku Akitapatapa Kutafuta Pumzi.

Atembezwa Mtupu

Wananchi wenye Hasira Kali Walianza Kumvamia kwa Kumpiga Bila Huruma na Kufanikiwa Kumvua Nguo zake na Kuanza Kumtembeza Barabarani. Hii Ni Aibu Kubwa Kuwahi Kuipata dada huyo Ambapo Wengi wamelihusisha Tukuio Hilo na Dhamira ya Kufanya Vitendo vya Kishirikina.

Kajala Aelezea Alivyonusurika Kifo baada ya Kunywa Kitu Chenye Sumu Hapo Jana.

Kajala
Kajala ni miongoni mwa waigizaji wa Tanzania ambao wamekua wakimake headlines mara kwa mara nchini Tanzania.
Screen Shot 2014-02-24 at 9.27.26 PM
Z

Wagoni Wapigwa Mawe hadi Kufa Huko Pakistan..

Wagoni

Wagoni Wauawa kwa Mawe.

Wagoni wawili Wanaokadiriwa kuwa na Miaka 30 kila mmoja Wameuwa Kikatili baada ya Kunaswa Wakishiriki Vitendo vya Ngono. Inasadikiwa Kuwa wagoni hao Kila mmoja na Ndoa yake na Kitendo cha Kunaswa Wakivunja Amri ya Sita Imewaghadhabisha Mno Raia wa Baluchistan Magharibi mwa Pakistan.
Aidha waliohusika na Mauaji ya Wagoni hao Wawili wamekamatwa na Polisi kwa Kosa la Mauaji, Baba na Kaka wa Mwanamke Pamoja na Mjomba wa Mwanaume wanashikiliwa na Polisi kwa Kosa Hilo la Mauaji.
Wagoni
Wagoni Wakiuawa kwa Kupigwa Mawe
“Ni kitendo cha Kikatili sana na Watu waliohusika na Mauaji haya ni Lazima Wafikishwe mbele ya Sheria” Alisema Bugti Ambaye ni Balozi wa Eneo Hilo la Magharibi mwa Pakistan

Hali ya Hatari.

Taarifa Zinaeleza Kuwa Kumekuwa na Ongezeko la Matendo ya Kinyama yanayofanyika Nchini Humo Hadi Kufikia Kiasi cha kesi 1000 kila Mwaka huku kukiwa na hofu ya Idadi Hiyo Kuzidi Kuongezeka Zaidi

MREMBO AFIA GESTI ARUSHA, CHANZO KIKIDAIWA KUWA USHIRIKINA...!! SOMA HAPA MKASA HUU...

MREMBO mmoja ambaye alihu-dumu kwenye nyumba ya kulala wageni na baa (jina tunalo) iliyopo Tengeru, wilayani Arumeru, mkoani Arusha, Blandina Michael (33) amekutwa amekufa kwenye moja ya vyumba vya nyumba hiyo huku chanzo cha tukio hilo kikihusishwa na vitendo vya ushirikiana.
Taarifa za awali zilimtuhumu mmiliki wa nyumba ya wageni moja ambaye pia anajihusisha na biashara za madini (jina tunalo) kwamba alimtoa kafara mhudumu huyo. Ilidaiwa kuwa, kila mwaka mtu mmoja katika biashara zake hupoteza maisha ghafla.
Hata hivyo, mfanyabiashara huyo alipoongea na Uwazi juzikati alikanusha vikali tuhuma hizo na kueleza kuwa yeye ni muumini mzuri wa imani yake.
‘’Hao watu wanapotosha sana, unajua kuna mwaka mwanaume mmoja alikufa ghafla kwenye nyumba yangu ya kulala wageni, alikuja na mpenzi wake ila alimeza Viagra ambazo hata polisi walizikuta mezani.
“Sasa watu wasio na nia njema na mimi tukio hilo wanaliunganisha na hili kwamba nawatoa kafara,” alisema.
Kifo cha Blandina kilitokea ndani ya chumba huku mtu mmoja anayedaiwa kuwa mpenzi wake aliyejulikana kwa jina moja la Timo, mkazi wa eneo hilo akihojiwa na polisi.
Marehemu Blandina ambaye ni mzaliwa wa mkoa wa Tanga, anaelezwa na bosi wake huyo kwamba alikuwa kama mtoto wa familia yake kwa vile alimwamini sana. Alifanya kazi hapo kwa miaka 8 na hakuwa na tatilo la kiafya.
Bosi huyo alisema mwili wa marehemu uligundulika baada ya mfanyakazi mwenzake wa kiume kumpigia simu saa 2 asubuhi ambapo simu yake ilikuwa ikiita bila kupokelewa ndipo alipoamua kwenda kumgongea katika chumba hicho.
Alisema baada ya kufika alishangaa kukuta mlango wa chumba chake uko wazi na alipochungulia alibaini kwamba Blandina alikuwa amefariki dunia.
Hata hivyo, polisi baada ya kufika na kuufanyia uchunguzi wa awali mwili huo hawakugundua kuwepo kwa jeraha lolote linaloashiria kuuawa, ingawa mwili huo ulipelekwa kufanyiwa uchunguzi wa kitaalam katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru.
Jeshi la Polisi mkoani Arusha limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali hiyo.

HUYU NDIYE MZUNGU ALIYEKAMATWA NA KILO 5 ZA MADAWA YA KULEVYA UWANJA WA NDEGE DAR-ES-SALAAM

Raia wa Henellic, Alexamdrios Atanasios, amekamatwa maafisa wa usalama wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam Jumapili usiku Februari 24, 2014, akiwa na kilo tano za madawa ya kulevya.

Habari zinasema mzungu huyo alikamatwa wakati wa upekuzi, akijiandaa kupanda ndege ya Swiss air kueleke jijini  Zurich, Uswisi.
Madawa hayo yalikutwa yakiwa yamefichwa kwenye “sakafu” ya begi lake baada ya mitambo ya kisasasa yaupekuzi, kugundua kuwa kulikuwa na ‘mzigo’.
Habari zinasema, kwa sasa mtuhumiwa anashikiliwa kwenye kituo cha polisi cha uwanjani hapo  akisubiri taratibu za kisheria ili afungukliwe mashtaka.

PICHA ZA UTATA ZA RIHANNA AKIWA NA MDOGO WAKE WAKIOGELEA....!! BOFYA HAPA KUZITAZAMA..

http://theclicktz.com/
Ki bongo bongo we na dada yako mnaweza kufanya hivi..?

http://theclicktz.com/

http://theclicktz.com/
Rihanna na Mdogo Wake Rajad

http://theclicktz.com/

Rihanna mkumbatia mdogo wake Rajad kwa mahaba hatarii sana

AFUNGWA KIFUNGO CHA MAISHA KWA KOSA LA KUMNAJISI MTOTO...!!

MKAZI wa mtaa wa Nsemulwa, Athuman Mussa (54) amehukumiwa kifungo cha maisha jela na Mahakama ya Wilaya ya Mpanda, baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kumnajisi mtoto wa kike mwenye umri wa miaka minne mdomoni.


Hukumu.

Hukumu hiyo ilitolewa juzi na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Chiganga Ntegwa baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na upande wa mashitaka uliongozwa na Mwendesha Mashtaka, Mkaguzi wa Polisi, Ally Mbwijo.
Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, mshtakiwa anadaiwa kutenda kosa hilo Juni 26 mwaka jana saa 12:00 jioni nyumbani kwake katika mtaa wa Nsemulwa katika Mji wa Mpanda.

Kumnajisi Mtoto

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Ntengwa alieleza kuwa siku hiyo ya tukio mshitakiwa alimkuta mtoto huyo ambaye wazazi wake ni jirani zake akiwa anacheza na watoto wenzake karibu na nyumba yake akamwita na kuingia naye ndani akiahidi kumpatia zawadi ya pipi aina ya jojo.
Baada ya mtoto huyo kuingia ndani ya nyumba, Athumani alimvuta kwenye kochi sebuleni na kisha alimwingizia uume wake kwenye mdomo wa mtoto huyo hadi hapo alipomaliza haja yake kisha akamwamuru aondoke nyumbani kwake ndipo mtoto huyo alipotoka mbio na kurejea kwao akilia.

 Kumnajisi
Aliiambia mahakama baada ya mtoto huyo kufika nyumbani kwao mama yake alimuuliza kilichomfanya alie ndipo alitema mbegu za kiume ambazo zilikuwa mdomoni mwake na kisha alimwelezea mama yake kila kitu alichotendewa na mshitakiwa.
Baada ya mama kuelezwa unyama huo wa Kumnajisi mtoto wake, naye alianza kulia kwa nguvu na kusababisha majirani kufika nyumbani hapo ambapo walielezwa alichofanyiwa mtoto huyo ndipo majirani walikwenda nyumbani kwa mshitakiwa wakamkamata na kumfikisha kwenye kituo cha polisi Wilaya ya Mpanda Jijini DAR.
Source: Habari L

Ajali mbaya ya malori yatokea mjini morogoro... mmoja wa dereva afariki dunia......

TAARIFA zilizotufikia hivi punde kutoka Morogoro ni kwamba malori mawili yamegongana eneo la Mikese mkoani humo na kulipuka moto ambapo mojawapo ya lori lilikuwa na shehena ya mafuta! Mpaka sasa malori hayo yanaendelea kuteketea kwa moto, na dereva mmoja wa lori amefariki. Taarifa zaidi na picha za tukio hili vitawajia punde!
>>>gpl

KWA HABARI ZILIZOTUFIKIA HIVI PUNDE: IKULU YA RAIS SOMALIA YASHAMBULIWA...

Al Shabaab
Wapiganaji wa kundi la wanamgambo la Al Shabaab nchini Somalia meshambulia Ikulu ya Rais katika mji mkuu Mogadishu.
Umoja wa mataifa unasema umefahamishwa kuwa rais wa nchi hiyo hakujeruhiwa na yu salama na kwamba shambulizi la wanamgambo hao lilitibuka.
Waziri wa mambo ya usalama wa nchi hiyo Abdi Karim Hussein, amesema baadhi ya washambuliaji wamefariki na wengine kukamatwa.

Kundi la Al- Shaabab linalopigana na utawala nchini humo limedai kuhusika na shambulio hilo na kusema makabiliano yangali yanaendelea.

Walianza mashambulizi yao, kwa kutumia gari lililokuwa na bomu ndani yake kwa kuliegesha kando ya ukuta na kisha kuanza kupigana ili kuweza kuingia ndani.

Milipuko mikubwa ilisikika pamoja na milio ya risasi.
Majeshi ya muungano wa Afrika yamekuwa yakipambana na wapiganaji hao na hata kuwafurusha kutoka mji mkuu Mogadishu. Hata hivyo bado wanadhibiti sehemu nyingi nje ya Mogadishu

VURUGU,FUJO... !! HIVI NDIVYO JINSI MSANII JAGUAR KUTOKA KENYA ALIPOAMUA KUMWAGA PESA KWA MASHABIKI WAKE NDANI YA CLUB..



Msanii kutoka 254 Kenya Jaguar katika show ya Nax Mingle iliyofanyika Nakuru, wiki iliyopita alimwaga mahela kwa mashabiki waliokuwa wamehudhuria show hiyo. Alitoa burungutu la pesa na kumwaga kwa mashabiki wake ambao chupuchupu wamuangushhe kutoka kwenye stage










MATAPELI YATUMIA MGAHAWA WA FRESH COACH MJINI MOSHI KUTAPELI MILIONI 5...

Mwanamke mmoja ambaye alifahamika kwa jina la Rashushi Amani Shembusho, mkazi wa Pasua, wilaya ya Moshi, mkoani Kilimanjaro, ametapeliwa kiasi cha shilingi milioni 5.4 na watu wasiojulikana asubuhi ya leo, Februari 20. 
 
Bi. Shembusho akilia kwa uchungu baada ya kudangasnywa na watu wawili, wa kike na wakiume ambao majina yao bado hayajafahamika. watu hao walimpeleka katika Hoteli maarufu mjini moshi, Fresh Coach na kumtapeli shilingi milioni 5.4 ambazo alikuwa ametoka kutoa Benki ya Uchumi ya mjini Moshi. 
 
Askari wa Hoteli hiyo inayodaiwa kutumika kumtapeli mwanamke huyo akimtuliza Mama huyo ambaye alionekana kuchanganyikiwa na tukio hilo.
 
Mama akilia kwa uchungu. 
 
Msamaria Mwema aliyefika katika eneo la tukio na kujitolea kumpeleka Mwanamke huyo katika kituo cha Polisi cha Kati cha Mjini Moshi.
 
Mama akisimulia tukio zima kwa wananchi waliofika katika eneo la tukio baada ya kumsikia akipinga ukunga kuomba msaada. 
 
Msamaria Mwema aliyefika katika eneo la tukio na kujitolea kumpeleka Mwanamke huyo katika kituo cha Polisi cha Kati cha Mjini Moshi. 
 
Bi. Shembusho akipanda gari la Msamaria Mwema aliyejitolea kumpeleka Polisi kutoa taarifa hizo. Na Dixon Busagaga wa globu ya jamii Moshi.

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. BONGONEWS TZ - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger