Showing posts with label Wema. Show all posts
Showing posts with label Wema. Show all posts

HII SASA IMEKUWA SIO KIFICHO TENA...!! TAZAMA KAMERA ILIVYO WAFUMA DIAMOND & WEMA WAKILA BATA USIKU WA JANA...


Hii ndo habari ya mujini......Wacha movie iendeleeeeeeeee.............
-jestina-george



MSIKILIZE JOKATE AKIELEZA JINSI ALIVYO MALIZA BEEF NA WEMA..NA KUMSAPRISE TSH.LAKI 6 JUKWAANI ARUSHA ...AUDIO YAKE HII HAPA..

Jokate Mwegelo aka Kidoti ameelezea jinsi ilivyokuwa mwishoni mwa wiki iliyopita, baada ya kumsurprise Wema Sepetu kwenye show ya msanii wake, Mirror iliyofanyika jijini Arusha.page
“It was a surprise,” Jokate ameiambia Bongo5. “Alinialika two weeks ago lakini sikuwa na uhakika kama ntaweza kwenda kutokana na ratiba zangu lakini later on nikasema ngoja nisimjibu, sikuongea naye tena kitu chochote. Kwahiyo nikaamua mimi na rafiki zangu kwenda Arusha, nikaamua tu
kumsuprise. Hakujua kama tupo wala sikusema popote kwamba naenda,”ameongeza Jokate.
cbf9c9f88cc911e38e2912d966ff09f8_8
Wema na Jokate wakiwa kwenye show ya Mirror jijini Arusha
“It was crazy,” amesema Jokate kuelezea ilivyokuwa baada ya yeye kupanda jukwaani. “It was nice though, kila mtu aliappreaciate, nadhani hicho ndio kitu kilichokuwa muhimu. I was also a bit nervous, sijawahi kufanya kitu kama kile na sikujua watu wataipokeaje but it was great. Kila mtu alifurahi, nadhani tumeipa pia heshima show yake.”
499b368c8cdc11e3b554122b944cbca2_8
Wema na Jokate wakicheza muziki pamoja
Jokate amesema yeye na Wema walikuwa wameshaziweka tofauti zao muda mrefu kuanzia kipindi kile kwenye msiba wa baba yake Wema, mwishoni mwa mwaka jana.
“Kwasababu ulikuwa msiba sikuweza kuweka public kwasababu msiba ni kitu sensitive sio vizuri kuchukua advantage kufanya vitu vingine ambavyo havieleweki. Naweza kusema ile ndio ilikuwa public appearance ya kwanza,” amesema Jokate.
8285c9ac8cce11e3931d0e6209f07faa_8
Jokate amesema hakuna tena tofauti kati yake na Wema na siku za usoni wanaweza kushirikiana katika mambo mengi ya kazi.
“I like it cause kuna wasichana wengi they look up to us. Tuangalie zaidi kushirikiana kuliko kuwa na vitu ambavyo havieleweki na havina mtazamo mzuri kwenye jamii. Na mimi hasa hicho ndio kilinisukuma kwamba do something kwenye event yake, kuonesha tu kwamba tunaweza kushirikiana na kufanya vitu positive kwenye jamii.”
Msikilize zaidi hapo chini.


 


WEMA, KAJALA, AUNT WACHAFUA HALI YA HEWA TRIPLE A JIJINI ARUSHA...TAZAMA PICHA HAPA WALICHOKIFANYA...

Kajala, Wema, Aunt na Zamaradi wakiwa katika pozi tofauti.
....Wakiwa pamoja na Mirror tayari kwa ajili ya kwenda kwenye Show, klabu ya  Triple A.
Wema Sepetu, Aunt Ezekiel na Kajala Masanja tayari kwa ajili ya kwenda ukumbini.
Kajala akipanda stejini.
Wema akipanda jukwaani huku akiacheza.
...Wakiwa katika picha ya pamoja.
...Wakicheza na Mirror.
Wema katika pozi.
Msanii Dyana Kimaro katika pozi.
Wema Sepetu pamoja na Meneja wake Martin Kadinda muda mfupi baada ya kuwasili jijini Arusha.
  

Wema Sepetu, Zamaradi na Martin Kadinda katika picha ya pozi.

Kajala Masanja na Aunt Ezekiel wakiwa wamepozi hotelini.

 MASTAA wa filamu Bongo, Wema Sepetu, Aunt Ezekiel, Kajala Masanja pamoja na wasanii wa Bongo Fleva Chid Benz na Miraji Hussein ‘Mirror’ hivi karibuni  walitinga katika jiji la Arusha kwa ajili ya kumtambulisha msanii Mirror kwenye klabu ya Triple A.

WEMA ANYANG'ANYWA KILA KITU, KISA KURUDIANA NA DIAMOND..

ZILE tambo, mbwembwe na majigambo ya Miss Tanzania 2006/07, aliye pia msanii wa filamu Bongo, Wema Isaac  Sepetu, zimefika mwisho kufuatia kunyang’anywa samani za ofisi yake ya Endless Fame Film Production na aliyekuwa mpenzi wake, Clement ‘kigogo wa ikulu’ na sasa amebaki mweupe.....
 

Wema Isaac  Sepetu.

 Kwa mujibu wa chanzo chetu, tukio hilo la aibu lilijiri hivi karibuni kwenye ofisi hiyo ya Wema iliyopo Mwananyamala-Komakoma jijini Dar
.
 KIGOGO WA IKULU AVAMIA NA MABAUNSA

Habari za uhakika zinadai kuwa, siku ya tukio, Clement akiwa ameongozana na watu waliosadikiwa kuwa ni mabaunsa, walivamia ofisi hiyo aliyomfungulia mlimbwende huyo na kukomba vitu vyote vya thamani alivyomnunulia wakati wa mapenzi motomoto (hakuna lenye mwanzo lisilo na ncha).

KUMBE ALIKODI CANTER

Kama njiwa apelekaye ujumbe muhimu wa huba, mtoa taarifa huyo alizidi kumwaga ‘upupu’ kuwa, siku hiyo Clement mbali na gari lake la kifahari, pia alitinga akiwa na gari aina ya Canter ambapo bila maswali wala maelezo achilia mbali ufafanuzi, alikusanya vifaa vyote na kuvirundika kwenye gari.
 
Wema akiwa katika ofisi yake kabla ya kunyang'anywa samani zilizomo.

IDADI YA VITU VILIVYOBEBWA

Vifaa hivyo ni tarakishi (computer), kamera ya kurekodi sinema (video camera), vifaa vya kurekebisha hali ya hewa (air conditioner), vifaa vya kuhifadhia umeme wa ziada, uninterruptible power supply  (ups) pamoja na vifaa vingine zikiwemo nyaya za umeme na kuiacha ofisi nyeupe kama uwanja wa mpira.

 “Hali ni mbaya sana, jamaa (Clement) alichukua kila kitu ndani ya ofisi hiyo kuanzia kompyuta, kamera hata nyaya! Hivi tunavyoongea, ofisi haina kitu kabisa,” kilisema ‘kikulacho’ hicho.

 CHANZO NI DIAMOND

Mpashaji huyo alizidi kuyapa utulivu masikio ya mwandishi wetu kuwa, chanzo cha kigogo huyo kufanya ‘umafia’ huo ni kitendo cha Wema kurejesha penzi lake kwa ‘mtemea maiki’ wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul Jumaa ‘Diamond Platnumz’.
 
Ofisi ya Wema kwa ndani.

 Taarifa hizo zilieleza kuwa, kitendo hicho kilichochea hasira za Clement, hasa pale Diamond alipohojiwa kuhusu kuingilia penzi hilo na kujibu hamwogopi mtu, “ndiyo maana Clement akaamua kumwaga ugali baada ya wawili hao (Wema na Diamond) kumwaga mboga,” kiliongeza chanzo.

HEBU MSIKILIZE WEMA

Ili kujua yapi ni maziwa na lipi ni tui juu ‘niuz’ hizo, mwandishi wetu alimtafuta Wema na kukutana naye laivu juzi ambapo alikiri kukumbwa na zahama hiyo huku akionesha mshangao wa wazi kwa kitendo alichofanyiwa na ‘zilipendwa’ wake huyo.
 

Geti la kuingia katika ofisi hiyo.

 “Ni kweli kabisa Clement amefanya hivyo, lakini nashangaa na ni mara yangu ya kwanza kuona wapenzi wakiachana mwanaume anaamua kuchukua vitu vyote alivyowahi kumnunulia au kumpa.
“Huo ni ushamba na unyanyasaji, akumbuke kwamba alipokuwa na mimi alinitumia pia,” alisema Wema na kuongeza:

 “Hata hivyo, namshukuru Mungu, vitu vyote alivyochukuwa Clement, baby (Diamond) kasema ataninunulia, wiki mbili hazitapita.”

Wema alikwenda mblele zaidi kwa kuonesha machungu yake kwa kigogo huyo pale aliposema: “Kwanza nasikia vitu vyenyewe alipofika nyumbani kavimwaga nje maana ndani hakuna nafasi.”
Wema akiwa na mpenzi wake Diamond aliyesababisha mpaka akanyang'anywa samani hizo.

KAANZA MWAKA VIBAYA

Mwanzoni mwa mwaka huu, Wema alikumbwa na mkasa wa kunyang’anywa lile gari la kifahari alilodai ni lake, Audi Q7 baada ya kusemekana kuwa halikuwa lake.

Kumbe gari hilo alipewa na Clement ambaye naye alilikopa kwa thamani ya shilingi milioni 90 kutoka kwa mtu aliyejulikana kwa jina la Shadrack Tweve.

 Tweve, baada ya kuzungushwa sana kulipwa fedha hizo, alikimbilia Mahakama ya Wilaya ya Ilala ambapo hakimu aliamuru gari hilo likamatwe na kurejeshewa mlalalamikaji huyo.

 PENZI LA WEMA, KIGOGO WA IKULU

Uhakika ni kwamba, penzi kati ya Wema na kigogo huyo halipo tena na kwa sasa jamaa ana demu mwingine (jina tunalo) ambapo mapaparazi wetu wanaendelea kufuatilia kwa karibu ili kuwanasa katika mazingira yoyote yale.

CREDIT: GPL

DIAMOND KAMPA MIMBA WEMA SEPETU?SOMA HAPA UJE UKWELI WA JAMBO HILI

MSANII maarufu wa Bongo Movie, mrembo na mwenye pesa pengine kuwazidi wengi na ambaye hivi karibuni amezua mijadala mikubwa baada ya kurudiana na mpenzi wake wa zamani Diamond, ambaye pia ni maarufu katika muziki wa kizazi kipya nchini na mwenye kuongoza kwa mapato nchini, imegundulika kuwa ana ujauzito wa miezi kadhaa.
Wema ambaye alishindwa kuficha hisia zake na hatimae kuweka kuandika kwenye mtandao wa kijamii wa instagram,” …mmmmmh jamani hichi kitumbo… hakifichiki now…” kuashiria kuwa mabadiliko ya mwili yameshaanza kuonekana (Picha chini inaonesha ujumbe huo kamili).

Mtandao wa huu ulianza kuhisi taarifa hizo na kuamua kuzifuatilia kwa karibu ili kujua nini haswa kinaendelea au ni hisia tu. Ndipo mwandishi alipochukua jukumu la kumtafuta mlimbwende huyo Wema Sepetu na kugonga mwamba.

Hata hivyo jitihada hizo hazikuishia hapo ndipo kilipopatikana chanzo cha karibu na Wema na kudai kuwa “ amekuwa akilalamika mabadiliko hayo na hata kusikika akisema anaihisi ameconsive…” kilisema chanzo hicho bila kutaka kutambulika hadharani.
“Ni kweli itakuwa hivyo na ndio maana Diamond aliamua kumtangaza rasmi siku hile ya chrismas” aliongeza.

Diamond ambaye alimtupilia mbali mpenzi wake Penny na kurudiana na Wema mapenzi yao hayakufichika kwani wakiwa China walipiga picha za mahaba na kuziweka kwenye mitandao ya kijamii na kuzua hisia tofauti.

Hivi karibuni wamekuwa karibu sana kimapenzi na kuamua kuonesha siri zao za ndani bila kuficha, “mwenye macho haambiwi ona… juzi tu wameweka video zao wakiwa kitandani kila mtu ameziona, lakni pia Diamond kumnunulia nyumba baada ya kusikia mkataba wake umeisha na kwamba hautoongezwa, na mambo mengine kibao” kiliongeza chanzo hicho

“lakini tusubiri miezi tisa tu sio mingi na mimba huwahaifichiki bana tutaona

Wema Sepetu na Diamond wajirekodi wakifanya yao kitandani



Penzi lenye historia ya kushamiri, kumwagana na kurudiana limezidi kuchukua sura mpya, safari hii, Wema Sepetu  amenaswa akimrekodi video baby wake Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.

Chanzo cha  kuvuja kwa scene hiyo mpya ilitokea Ijumaa iliyopita ambapo bila hiyana, bibie Wema aliamua kuitupia video katika Mtandao wa Instagram ambayo alimrekodi Diamond aliyekuwa akiandika mashairi kitandani, akamsumbua kwa kumrekodi huko na kusindikiza kwa ujumbe uliosomeka:
 
“In da middle of his writing session…just had to disturb him a little”(Katikati ya muda wake wa kurekodi...nikamsumbua kidogo).
 
Diamond aliyekuwa akiandika mashairi, alisumbuliwa na Wema kwa kumrekodi huku akimtaka aweke mapozi tofautitofauti hali iliyomfanya ‘boyfriend’ wake huyo waliyerudiana siku chache zilizopita, apoteze umakini wa kuendelea kuandika mashairi.
 
Baada ya muda mfupi, ‘posti’ hiyo ya Wema ilipata maoni kibao huku kila mmoja akiweka mtazamo wake. Kuna ambao walimpongeza kwa kufurahi kuona uhusiano wao huku wengine wakiponda kuwa wamechoka ‘drama’ zao za kila siku.

VIDEO IKO HAPO CHINI 

BAADA YA WEMA NA DIAMOND KURUDIANA..!! KIGOGO WA WEMA ATANGAZA VITA NA DIAMOND...SOMA ZAIDI HAPA..

YULE kigogo au taita aliyekuwa akimpa jeuri ya fedha Wema Isaac Sepetu ajulikanaye kwa jina moja la Clement anadaiwa kutangaza vita na staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul Jumaa ‘Diamond Platnumz’.

Habari ‘hoti’ zinadai kuwa Clement anataka Diamond arudishe gharama alizomgharamia Wema ndipo waendeleze mapenzi yao.
Nasibu Abdul Jumaa ‘Diamond Platnumz’ na Wema Isaac Sepetu katika pozi.
Kwa mujibu wa mtu wa karibu wa kigogo huo, Clement anadai kwamba gharama alizotumia kwa Wema ni kubwa mno lakini bidada hakujali chochote na kuukabidhi moyo wake kwa ‘Mtoto wa Tandale’ ambaye ndiye barafu wa moyo wake.
Wema Isaac Sepetu.
“CK (Clement) anaumia sana kuona kuwa ameteketeza fedha nyingi kwa Wema lakini bila hiyana, mrembo huyo akabwaga manyanga kisha akarudisha mpira kwa kipa na kuanza moja huku kaka mkubwa akiachwa kwenye mataa,” alitonya mnyetishaji huyo bila kufafanua kama Clement aliachwa mataa ya eneo gani.

Akiendelea kutiririka bila kuweka nukta au ya mkato, mtu huyo alisema kuwa kiasi ambacho kinadaiwa kuteketea kwa Wema kinakaribia Sh. milioni 279.6 ambazo gharama hizo zinahusisha vitu kadhaa alivyowekeza kwa Wema.

“Kuna gharama za utengenezaji wa Filamu ya The Super Star ambayo haijulikani kilichotokea kwani hadi leo haionekani sokoni.

“Kama hiyo haitoshi kwenye uzinduzi wa filamu hiyo akamleta staa wa filamu wa Nollywood, Nigeria, Omotola Jalade Ekeinde na sherehe mbili za uzinduzi zilifanyika katika hoteli kubwa mbili tofauti, ikasemekana milioni arobaini na nane ziliteketea.
 
Nasibu Abdul Jumaa ‘Diamond Platnumz’.
“Kuna kodi ya pango la ofisi ya Wema ya Endless Fame iliyopo Mwananyamala Koma-koma, Dar, jamaa alilipa milioni nane na laki nne kodi ya miaka miwili ambayo kwa mwezi ni laki tatu na nusu.

“Ukiachana na gharama za nyumba na ofisi, kuna gari aina ya Audi Q7, inadaiwa kanunua Clement kwa Sh. milioni 98, Toyota  Harrier Lexusya Sh. milioni 48 na Toyota Mark X iliyomtoa Sh. milioni 25.

“Usisahau hata lile Toyota Noah ‘kitimoto’ la ofisi alinunua Clement kwa Sh. milioni 10, faini aliyolipiwa Kajala Masanja mahakamani Sh. milioni 13, gharama za kuirekebisha ngozi yake alipoenda nchini China iligharimu Sh. milioni 14, yaani jumla ni kama Sh. milioni 279 na ushee. Na hiyo ni kwa vitu vinavyojulikana ukiachia mbali shopping za Dubai,” alitiririka kikulacho huyo.

Baada ya kujazwa data, Paparazi wetu alijaribu kumtafuta kigogo huyo lakini licha ya juhudi zote hizo hakuweza kupatikana ndipo alipogeukiwa Diamond:

 “Sitishiki kwa lolote lile kwani huko nyuma kabla sijawa maarufu kivile enzi ya Nenda Kamwambie (wimbo) niliwahi kukaa mahabusu kwa siku kadhaa na sababu ilikuwa mapenzi kwa hiyo kwa hili siogopi kitu kwanza mimi ndiyo alinichukulia na mwana mpotevu amerudi kundini,” alisema Diamond anayekimbiza na Ngoma ya Number One.

"Siri ya mafanikio yangu ni Martin Kadinda...Yeye ndo mtu pekee aijuaye siri ya mafanikio yangu"...Wema Sepetu


MSANII nyota wa filamu Bongo Wema Isack Sepetu amefunguka kwa kudai kuwa hawezi kuvunja urafiki na meneja wake Martin Kadinda kwa sababu kama kuna kitu chochote cha mafanikio nyuma yake yupo Kadinda.

Wema Sepetu ameuambia mtandao wa FilamCentral  kuwa hana rafiki anayejua siri zake zaidi ya meneja huyo ambaye amekuwa akimuongoza vema.

“Kadinda ndo kila kitu kwangu, hata akiondoka na kukaa mbali na mimi kwa muda mrefu ninapokutana naye tu, nitamweleza kila kitu toka siku ya mwisho tuliyoachana, hivyo inakuwa kama sijapoteana naye,yaani ni kama vile nipo naye kila siku iendayo kwa Mungu,”anasema Wema.
 
Msanii huyu ameendelea kusema kwamba hata kampuni yake ya Endless Fame film aliifungua kwa msaada wa Kadinda baada ya kumshauri  kuwa kwa hadhi yake anastahili kuwa na kampuni na aache kuigiza filamu za watu wengine.

BAADA YA WOSIA WA MAREHEMU BABA YAKE WEMA KUSEMA WAZI ....WEMA NA DIAMOND WATANGAZA RASMI NDOA


HUKU mchumba’ke, Penniel Mungilwa ‘Penny’ akifungasha virago kurejea kwao, mzee mzima Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ametangaza kumuoa Miss Tanzania 2006, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’. 

Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’(kushoto) na Penniel Mungilwa ‘Penny’ wakiongea jambo enzi za mapenzi yao.
Ishu hiyo ilijiri ndani ya Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar ambapo mkali huyo wa Bongo Fleva alikuwa akikamua kwenye sherehe ya Krismasi aliyoiandaa mwenyewe. 
Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ baada ya kupanda jukwaani katika viwanja vya leaders.
TANGAZO LA AWALI
Awali kabla ya kufikia eneo la kutangaza kuoana, Diamond aliweka wazi jukwaani kwamba yeye na Wema wamerudiana. Diamond Platnumz akiongea jambo baada ya Wema Isaac Sepetu ‘Madam’  kupanda jukwaani.
MTIRIRIKO ULIVYOKUWA
Diamond, akiwa ameshika kipaza sauti alikatisha kuimba na kuwauliza mashabiki wake, hasa watoto waliohudhuria kwa wingi tamasha hilo, je, wanataka kumuona shemeji yao?
“Itakuwa si vizuri mkaondoka bila kumuona shemeji yenu, nikuleteeni mumuone?” aliuliza  Diamond. Swali hilohilo akalirudia tena ambapo lilipokelewa kwa shangwe huku mashabiki wakilitaja jina la Wema.                                         Diamond Platnumz na Wema Isaac Sepetu wakijiachia.
WEMA APANDISHWA JUKWAANI
Kufuatia kelele za mashabiki, Diamond alimuomba Disco Joker (DJ) wake amuwekee Wimbo wa Ukimwona ambao ulisindikiza ujio wa Wema jukwaani akifuatana na wapambe wa Diamond.
“DJ acha huo, nipigie Wimbo wa Ukimwona watu wangu wa nguvu wamwone shemeji yao kwani tangu nilivyokwenda naye China walikuwa wakisumbuliwa na maneno tofautitofauti kutoka kwenye mitandao ya kijamii,” alisikika Diamond.
 Diamond, akiwa ameshika kipaza sauti akiima Wimbo wa Ukimwona na Wema akiwa amemkumatia.
JUKWAA SASA
Hali haikuwa ya kawaida jukwaani kwani kilichofuata hapo ni Wema kuonesha kwa vitendo mambo yaliyoashiria kuwa, wawili hao sasa ni mwendo mdundo.
Wema alishuhudiwa akimzungushia mikono Diamond kwenye kiuno jambo ambalo liliwafanya baadhi ya mashabiki wa mastaa hao kutoa machozi ya furaha kuona penzi la wawili hao limerudi upya, wengine walimwambia Diamond amuoe Wema.
“Diamond muoe Wema, mnapendezana sana,” walisikika mashabiki.


Wema Isaac Sepetu ‘Madam’akimuaga Diamond Platnumz kwa kumkumatia.
MAWIFI WADAI KUHARIBIWA SIKU NA KAKA YAO
Hata hivyo, kitendo cha Diamond kumwita Wema jukwaani kilionekana kuharibu furaha ya sikukuu kwa ndugu zake kwani bila ya kuuma midomo dada zake staa huyo wakiongozwa na Esma Khan walinuna na kuanza kuondoka.
“Yaani siku yangu imeshaharibika, nilikuja nina furaha sasa imepotea, tuondokeni ndugu zanguni,” alisema Esma akiwaambia Mwanaisha Abdul ‘Queen Darleen’ na Halima Haroun ‘Kimwana’.
 

Diamond Platnumz na Penny wakiwa pamoja enzi za mapenzi yao.
MAMA DIAMOND ASHANGAA
Kitendo cha ndugu hao kukasirika hakikupokelewa vizuri na bi mkubwa wao yaani mama Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra’ ambaye aliwajia juu akiwashangaa.
“Wajinga nini? Sasa walitaka Diamond… (tusi) wao, mtu ameshaamua kupenda wamwache, mi’ mwenyewe nimeshajifunza, sitaki kuingilia penzi lake,” alisema mwanamke huyo ambaye mjini anazungukia usafiri aina ya Altezza.


Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’  na Penniel Mungilwa ‘Penny’.
Baada ya shoo hiyo iliyomalizika saa moja usiku, paparazi wetu alimfuata Diamond akiwa amesimama na Wema na kuwauliza kama kweli wana nia ya kufunga ndoa.
“Hilo mwana mbona lipo wazi, nataka kumuoa staa na nataka kuzaa na staa,” alisema Diamond huku Wema akiwa hapingi.
 
MAMA WEMA ATANGAZA VITA  NA DIAMOND
Wakati Dimaond akitambia ndoa na Wema, siku hiyohiyo ya Krismasi, mama wa Wema, Mariam Sepetu alidaiwa kutangaza vita na mwanamuziki huyo baada ya kusikia tetesi kuwa amerudiana na mwanaye.
Kwa mujibu wa rafiki wa karibu wa mama Wema (jina tunalo) mama wa staa huyo alichukizwa na kitendo cha Diamond kurudiana na mwanaye kwani anaamini anamchezea tu.


 
Mama wa Wema, Mariam Sepetu.
Rafiki huyo alizidi kudai kuwa, taarifa hizo zimemuweka  mama huyo kwenye wakati mgumu na kudai kuwa popote atakapokutana na mwanamziki huyo atampopoa mawe au machungwa hata ikiwa siku ya ndoa yao.
“Mama Wema amesema hampendi Diamond, popote atakapomuona itakuwa vita ya wawili, kama kuna jiwe atamrushia, hata machungwa kama yapo yatakuwa halali yake,” alisema rafiki huyo.
 
WOSIA WA MZEE SEPETU
Mpashaji huyo wetu alizidi kufunguka kuwa, mama Wema ana wosia mkononi ambao aliuacha marehemu mumewe, mzee Isaac Abraham Sepetu.
Alisema katika wosia huo, mzee huyo alisema hataki Diamond amuoe Wema na kama mrembo huyo atakiuka  wosia huo atapatwa na laana mbaya katika maisha yake.
Kinachomuumiza zaidi mama Wema ni huo wosia, mzee Sepetu alisema hataki mtoto wake aolewe na Diamond, kama atakataa kuna kitu kibaya kitamkuta katika maisha yake,” alisema rafiki huyo.
 
MAMA WEMA ASAKWA
Baada ya kupata habari hizo, gazeti hili lilimvutia waya mama Wema ili kuweza kuthibitisha madai hayo ambapo alisema kuwa, hayuko tayari kuzungumzia jambo hilo kwa wakati huo mpaka atapoamua akisisitiza muda si mrefu.
Jamani nina mambo mengi sana ya kufanya na sijatulia kabisa siko tayari kuzungumza chochote kwa sasa nikiwa tayari nitawaambia kila kitu,” alisema mama Wema.

SNURA AMWAGIA SIFA KIBAO WEMA SEPETU.NI BAADA YA KUHUSIKA KWENYE VIDEO YAKE YA NIMEVURUGWA

clip_image001Hatimaye baada ya ukimya mrefu kuhusu urafiki wao, leo hii Snura ameamua kufunguka, na kukumbuka fadhila na ukarimu wa Wema kwake kipindi cha nyuma na hasa alipotoka mara ya kwanza kabisa kimuziki. Kupitia ukurasa wake wa Instagram mwimbaji huyo wa NIMEVURUGWA ame andika kifuatacho:clip_image001clip_image001[5]Hakuna kitu kizuri kama kushukuru na kukukumbuka fadhila no matter what. Well done Snura.

"Siwezi kushindana na DIAMOND kwasababu mimi sio Mwimbaji"...WEMA


Je wewe ni kati ya wanaoamini kuwa wapenzi ‘wa zamani’ Wema Sepetu na Diamond Platnumz wanashindana kwa namna yoyote? Star wa kipindi cha ‘In My Shoes’ Wema Sepetu ameshare ujumbe kwa wote wanaofikiria hivyo.

Kupitia Instagram ameandika kuwa kitu pekee kinachosababisha watu wahisi hivyo ni kutokana na wote wawili kuwa na mafanikio katika fani zao (muziki na movie), na kuongeza kuwa hawezi kushindana na Diamond sababu yeye sio muimbaji. 

Source: Bongo 5

WEMA ALIMISS PENZI LA DIAMOND.SOMA HAPA ZAIDI....

Mcheza filamu za kibongo Wema Sepetu ametuma picha ya mpenzi wake wa zaman mwanamuziki Diamond Platnamu kwenye akaunti.yake ya instagram na kuandika,

“ i jus happen to love dis picture

baada ya kuweka picha hiyo mashabiki wameanza kumsifia uku wakimponda mpenzi Penny ambae anaaminika ndio mpenzi wa Diamond kwa sasa
Website hii imepitia akaunti ya Diamond na kukuta picha ile ile aliyoweka Wema ikiwa na maneno kuonesha kua usiku wa jana msanii huyu alikua kwenye sherehe ya kuzaliwa mrembo wa zamani wa Tanzania Jackline Ntuyabaliwe.




Y
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. BONGONEWS TZ - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger