Showing posts with label LULU. Show all posts
Showing posts with label LULU. Show all posts

DIVA WA CLOUDS: NAMPENDA SANA LULU, NINGEKUWA MWANAUME NINGEMTONGOZA.....!! SOMA HAPA

Mwanadada Loveness aka Diva the Boss mtangazaji wa clouds fm kipindi cha ala za roho,kinachozungumzia maswala ya mapenzi na mahusiano…..Jana usiku alijikuta akielezea hisia zake kwa Muigizaji  Elizabeth Michel aka Lulu “Kutoka moyoni nampenda sana huyu binti, ningekuwa mwanaume ningemfuata na kumu approach, sema mimi  ni mwanamke tu”.
Hii ilikuwa kabla ya kucheza wimbo wa atatamani ambayo ni version  ilioimbwa Lulu. Wimbo halisi uliimbwa   na Linnah msanii kutoka THT

Back in days .Diva kupitia account yake ya instagram aliwahi kupost picha hii ambayo ilizua utata….sasa baada ya kumsikia  nikashindwa kumuelewa…Jionee mwenyewe…then achia comment!

credit : domozege blog


TAZAMA MATUKIO KATIKA PICHA:LULU AKIRI ALIKUA NA MAHUSIANO YA KIMAPENZI NA KANUMBA LEO MAHAKAMI...HIVI NDIVYO ILIVYOKUA


Kesi ya kuua bila kukusudia inayomkabiri muigizaji wa kike, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu imesikilizwa leo (February 17) katika mahakama kuu, Kanda ya Dar es Salaam.
 
Lulu alikiri mbele ya Jaji Rose Temba kuwa alikuwa na uhusiano wa mapenzi na marehemu Steven Kanumba na kwamba walikuwa na ugomvi, lakini alikana mashitaka ya kumuua bila kukusudia.
 
Mbali na kukiri kuwa na uhusianano wa mapenzi, muigizaji huyo pia alikiri kuwa baada ya tukio hilo alitoka nje ya chumba walichokuwepo na kwenda kumwambia mdogo wake marehemu Kanumba, Setti Bosco kuwa Kanumba ametangulia mbele ya haki.
 
Akisoma hati ya mashitaka, Wakili Mwandamizi wa Serikali, Monica Mbogo, alidai kuwa Aprili 7, mwaka 2012, Sinza Vatikani, Mkoa wa Dar es salaam, mshitakiwa alimuua bila kukusudia Stevin Kanumba.
 
Wakili Kombo, alidai kuwa pamoja na mambo mengine, marehemu Kanumba baada ya kufa, mwili wake ilipelekwa hospitali ya Taifa Muhimbili ambapo majibu yanaonyesha kwamba kifo chake kimesababishwa na uvimbe ndani ya ubongo.
 
Upande wa serikali una mashahidi watano pamoja na vielelezo wakati upande wa utetezi pia unatarajia kuwa na mashahidi watano na vielelezo.



MASKINI....LULU KESI UPYAA...!! SAFARI KESI KUSIKILIZWA KWA MUDA WA MIAKA MIWILI KABLA YA HUKUMU KUTOLEWA...

KAZI inaanza tena! Supastaa wa filamu za Bongo, Elizabeth Michael Kimemeta ‘Lulu’ anapanda katika kizimba cha Mahakama Kuu ya Tanzania kwa yale madai ya kumuua bila kukusudia, aliyekuwa nyota wa muvi nchini, marehemu Steven Charles Kanumba ‘The Great’, Risasi Jumamosi limeambiwa.
Supastaa wa filamu za Bongo, Elizabeth Michael Kimemeta ‘Lulu’.
Akizungumza na gazeti hili juzi jijini Dar es Salaam, mtoa habari ambaye aliomba hifadhi ya jina alisema kuwa, Februari 17, mwaka huu, staa huyo atatakiwa mahakamani hapo kwa ajili ya kesi yake kuanza huku akisema, kuna mabadiliko kidogo katika kusikilizwa kwa kesi hiyo.
Marehemu Steven Charles Kanumba ‘The Great’.
ITAKUWAJE?
Kwa mujibu wa mtoa habari huyo, Lulu mwenye umri wa miaka 18, atasomewa upya mashitaka dhidi yake ambapo atatakiwa kujibu tena kama anakubali aliua bila kukusudia au la!
“Elizabeth (Lulu) atasomewa upya mashitaka ya kumuua Kanumba bila kukusudia.
“Ataulizwa ni kweli au si kweli? Atatakiwa kujibu swali moja kati ya hayo mawili, kama ni kweli atasema kweli kama si kweli atasema si kweli,” kilisema chanzo hicho huku kikisisitiza jina lake lisichorwe gazetini.

MUDA WA KESI SIKU 730
Habari zaidi zikadondokea Dawati la Risasi Jumamosi na kusema kwamba, kesi hiyo itaendeshwa kwa siku mia saba na thelathini (730), kwa maana ya miaka miwili hadi hukumu itakapotolewa.

NI NDANI YA SHERIA MPYA
Katika Siku ya Sheria Duniani iliyoadhimishwa jijini Dar es Salaam, Februari 3, mwaka huu, Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed Chande Othman alisema kuanzia sasa kesi zote za jinai zitatakiwa kumalizika katika kipindi cha miaka miwili.
Kesi ya Lulu nayo ni ya jinai na kwa sababu hiyo, hadi Februari ya mwaka 2016 itatakiwa iwe imemalizika.
Wakili wa Lulu, Peter Kibatala.
WAKILI WAKE
Chanzo hicho kililithibitishia gazeti hili kwamba, Lulu atatetewa na yuleyule wakili wake mwenye ‘ngekewa’ ya kuwatetea watu maarufu nchini, Peter Kibatala.
Kibatala ameshawahi kuwa wakili wa Mbongo Fleva, Isaac Waziri Makuto ‘Lord Eyez’ katika kesi ya madai ya kuiba ‘power window’ za gari la msanii mwingine wa Bongo Fleva, Omary Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’.
Pia aliwahi kumwakilisha wakili mwezake, Mabere Nyaucho Marando kwenye kesi ya Mbongo Fleva, Judith Wambura ‘Jide’ alipoburuzwa kortini na uongozi wa Clouds Media Group baada ya Marando kuwa na udhuru.
Ilibaki kidogo awe wakili wa Miss Tanzania 2006, Wema Isaac Sepetu katika kesi ya kumpiga makofi meneja wa hoteli moja (jina tunalo) iliyopo Kawe Beach, Godluck Kuyumbu lakini akakosa sifa baada ya shauri hilo kusiklizwa Mahakama ya Mwanzo Kawe, Dar.

HAWA HUENDA WAKAITWA
Kwa mujibu wa mtoa habari wetu, katika kesi hiyo huenda wakaitwa watu ambao watasaidia kutoa ushahidi.
Watu hao ni wale waliokuwa na ukaribu na marehemu, hasa siku ya tukio au kushirikishwa kwa namna moja au nyingine kwa jinsi ambavyo waendesha mashitaka wataona.

DOKTA KIDUME
Aliyekuwa akimtibu Kanumba, Dokta Kidume anaweza kufika mahakamani hapo kwa sababu ndiye aliyekuwa mtu wa pili  kufika kwenye chumba cha marehemu mara baada ya kuanguka.
Mdogo’ wa marehemu Kanumba, Seth Bosco.
SETH BOSCO
Huyu ni ‘mdogo’ wa marehemu Kanumba, yeye siku ya tukio alikuwa nyumba moja na marehemu, ila vyumba tofauti. Ndiye aliyemwona Kanumba akiwa katika hali mbaya baada ya kutoelewana na Lulu na kukimbia kumwita Dokta Kidume.  
Hawa wote walishahojiwa na Jeshi la Polisi Tanzania katika Kituo cha Oysterbay, Dar, mara baada ya kifo hicho. Seth alihojiwa mara tano.

TUJIKUMBUSHE
Kanumba alifariki dunia Aprili 7, 2012 nyumbani kwake, Sinza jijini Dar es Salaam. Kifo chake kilidaiwa kilitokana na kuangukia sehemu ya nyuma ya kichwa na hivyo kuufanya ubongo kutikisika (brain concussion).
Hata hivyo, baadaye ilifahamika kuwa, sehemu ya maini na majimaji ya machoni vilipelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ili kubaini endapo kulikuwa na sumu au kitu kingine katika mwili wa Kanumba. Majibu hayajatoka hadi leo.

WAKILI KIBATALA
Risasi Jumamosi lilimsaka Wakili Kibatala kwa njia ya simu ili kumsikia alichonacho kufuatia kesi ya mteja wake kuanza kusikilizwa ambapo alisema:
“Tutakutana mahakamani jamani, kwa sasa niko bize sana.”

LULU
Juzi, simu ya Lulu ilipigwa kwa muda mrefu lakini haikupokelewa huku baadhi ya watu wake wa karibu wakisema kuwa, staa huyo ameasisi tabia mpya ya kutopokea simu zenye namba ngeni machoni mwake.
-GPL

KIVAZI CHA AJABU CHA LULU MICHAEL CHAZUA UTATA

Mavazi anayovaa msanii wa filamu Elizabeth Michael ‘Lulu,’ sasa yanamuweka matatani kufuatia hivi karibuni kushambuliwa kwa maneno kutokana na kigauni cha kimitego alichokuwa amevaa.

Kigauni hicho ambacho juzikati alionekana nacho mitaa ya Sinza jijini Dar kisha baadaye kukitupia mtandaoni, kimewafanya wengi wahoji anakoelekea msanii huyo anayedai amebadilika.lulu“Hivi huyu ndiye anayesema amebadilika kweli kwa mavazi haya, mbona anataka kuwapa wakati mgumu wanaume? Ndo ili iweje sasa, ama kweli jasiri haachi asili,” alisema mdau mmoja baada ya kuiona picha hiyo.

Ijumaa lilifanya jitihada za kumtafuta Lulu ili kujua sababu ya kuvaa mavazi hayo lakini simu yake iliita bila kupokelewa.
J

LULU APIGA BONGE LA MSAMBA MAZOEZINI,BINTI AMEIVA HII NI KWENYE HARAKATI ZAKE ZA KUONDOA MANYAMA UZEMBE






Kweli Mwanadada kaamua kupunguza mwili ...Huo msamba dahhhhhhh

Lulu Michael na Young D wafumaniwa wakifanya mapenzi ndani ya gari


 
Jana kupitia kwenye kipindi cha U-heard cha Clouds FM chini ya bwana Sudi Brown ama Gossip Cop kulikuwa na fununu kali iliyokuwa inamuhusu mwanadada wa Bongo Movies na mwimbaji wa muziki wa kizazi kipya Young D 'Young Dar es Salaam' kama mwenyewe anavyojiita baada ya wawili hao kukutwa kwenye gari wakifanya lile tendo linaloruhusiwa kufanywa mara baada ya mdada na mkaka kufunga ndoa.
                                                                              
Kwa mujibu wa Sudi Brown 'Gossip Cop' wawili hao walikutwa maeneo ya Mbezi Beach ndani ya gari aina ya Hyundai ya mwanadada Lulu na polisi wa doria wakivunja amri hiyo iliyokatazwa na vitabu vyote vitakatifu kwa maana ya biblia, Quran na vitabu vingine vya dini ulimwenguni.


Habari zaidi  zinasema baada ya wawili hao kukutwa eneo hilo na polisi walipelekwa pembeni gizani na kuongea na Polisi kabla ya wao kutokomea wasipojulikana na gari hilo.
 
Alipopigiwa simu mwanadada LULU alipokea na kukata muda mfupi na baadaye Young D alipopigiwa simu alitoa majibu ya utata kama alivyoongea mwenyewe kupitia kwenye kipindi cha U-heard cha Clouds Fm.
Bofya  hapo  chini   usikilize  mkasa  huo

LULU Awahamasisha vijana juu ya Upimaji wa Virusi vya Ukimwi...!!





Msanii wa filamu nchini Elizabeth Michael aka Lulu amesema vijana wanatakiwa wawe mstari wa mbele katika kujikinga na maambukizi ya virusi vya Ukimwi.
 
Akizungumza na mwandishi wetu jana katika usiku wa Red Ribbon Fashion Galla iliyofanyika Mlimani City jijini Dar es Salaam, Lulu alisema siku ya Ukimwi duniani inatukumbusha kuangalia tumetoka wapi na tunakwenda wapi na kuangalia wangapi wamepoteza maisha kwaajili ya gonjwa la Ukimwi.
 
Najumuika na Watanzania leo ,siku ya Ukimwi duniani ambayo hufanyika kila mwaka, kwa kuangalia wangapi wamepoteza maisha, pamoja na kuwahamasisha zaidi vijana Wakitanzania kutumia kinga ili kupunguza maambukizi ya virusi vya Ukimwi ambavyo vinapoteza nguvu ya Taifa,” alisema Lulu.
 
Pia Lulu alisema amekuwa akipima Ukimwi mara kwa mara ili kuangalia afya yake,huku akiwashauri vijana kwenda kupima ili kujua afya zao.
 
“Nimekuwa nikipima HIV kila mara katika hatua za maisha yangu,kuangalia kuhakikisha najiweka katika usalama wa afya yangu,pamoja na kupanga matarajio ya maisha.Sio kuwa ukipima ukagundulikana una HIV utashindwa kupanga malengo yako hapana! ukipata ushauri nasaha, ukajua uishi vipi kwa kuboresha afya yako, maisha yataendelea kama kawaida. Kwahiyo kinachotakiwa vijana ni kujua afya zetu mapema”

PICHA: LULU ATOA MSAADA WA FEDHA HOSPITALI YA OCEAN ROAD KWA WAGONJWA WA CANCER....


Mwanadada Elizabeth Michael ama LULU leo ametembelea hospitali ya Ocean Road Iliyopo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutoa zawadi za fedha kwa ajili ya wagonjwa wa cancer hospitalini hapo. kupitia ukurasa wake wa instagram LULU ameandika
"Naamini Mimi sio mwema sana mpk Mungu akaniwezesha kuona mwezi huu nikiwa mzima na mwenye afya...!kwa kutambua Hilo nimeanza mwezi huu kwa kupita ktk hospital ya OCEAN ROAD na kutoa mchango ili kuwasaidia wagonjwa wa CANCER...!Tuwe na utaratibu wa kuwakumbuka wahitaji kwa chochote tulichonacho! Nawatakia mwezi wenye Baraka na mafanikio!..." Hongera sana lulu kwa moyo wako huu. CREDIT : BONGOMOVIES

LULU APOROMOSHA MVUA YA MATUSI KATIKA MSIBA WA BABA YAKE WEMA SEPETU ...!

MSANII nyota wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amejikuta akiporomosha mitusi mizito ya nguoni kwenye msiba wa baba wa Miss Tanzania 2006/07, Wema Isaac Sepetu, mzee Isaac Abraham Sepetu hali iliyowafanya baadhi ya waombolezaji kumkodolea macho ya mshangao.
 
 Elizabeth Michael ‘Lulu’ akiwa msibani kwa marehemu Balozi Sepetu.
Tukio hilo lililotawaliwa na hasira lilijiri Oktoba 28, 2013 kwenye msiba huo uliokuwa ukiombolezwa nyumbani kwa marehemu, Sinza-Mori jijini Dar es Salaam.
KISA NA MKASA
Ilikuwa wakati Lulu akitinga msibani hapo, ghafla alimfuata mmoja wa waandishi wa habari hii na kuanza kumporomoshea matusi hayo kwa kile alichodai kukerwa na habari iliyowahi kuandikwa juu ya kitendo chake cha kula chakula sahani tatu katika hafla moja iliyofanyika hivi karibuni huko Kunduchi Beach Hotel, Dar.

TUJIKUMBUSHE KIDOGO
Katika tukio hilo la awali, Lulu alikuwa mmoja wa waalikwa wa harambee ya kuchangia kansa ya matiti kwa akina mama iliyofanyika kwenye hoteli hiyo.

Wakati wa chakula cha mchana kilichoandaliwa kwa ajili ya wachangiaji wote, Lulu alionekana akirudia kuchukua msosi kwa zaidi ya mara tatu (alikula sahani tatu).
TURUDI MSIBANI
Baadhi ya watu waliokuwa msibani hapo walimshangaa Lulu kwa kuporomosha matusi hayo ya nguoni wakati akijua kuwa yeye ni kioo cha jamii na baadhi ya maneno machafu aliyoyatamka hadharani hayaandikiki gazetini wala mtandaoni.

MSIKILIZE LULU
“Siwapendi nyinyi waandishi hasa wewe (akamtaja jina). ‘I don’t want your f**** story dude, go to hell with you’re f**** shit,” alisikika Lulu akitamka matusi hayo. (hatuwezi kuyatafsiri kwa sababu za kimaadili).

WAOMBOLEZAJI SASA
Mamia ya waombolezaji waliokuwepo eneo la msiba huo walionesha kushangazwa na kitendo cha binti huyo aliyejipatia umaarufu kutokana na kuigiza kwake.

Baadhi yao walidai hali hiyo haikuwa ya kawaida na huenda alikuwa ‘amepata kiburudisho’ (alikunywa pombe).
“Sasa binti si uende ndani ukakae? Hapa ni msibani halafu wewe unasema maneno kama hayo, huoni kama unasumbua akili za wenzako?” mzee mmoja alisikika akisema wakati Lulu anaondoka.

“Unajua hawa mastaa wa Bongo mimi nimeshawajua kwani nawafuatilia sana, wakiandikwa kwa mazuri meno thelathini na mbili nje, wakiandikwa kwa mabaya timbwili kama hili.
“Hiyo habari anayoilalamikia mimi niliiona kwenye gazeti tena ilikuwa na picha sasa alichokereka ni nini, si kweli au?” alisikika mwombolezaji mwingine.
Mwombolezaji mwingine alisema Lulu anaweza kuwa na hoja lakini inakufa kwa vile kama habari ilimkera alipaswa kumtafuta paparazi huyo kwa wakati wake au afike Ofisi za Global badala ya kujianika hadharani huku akidai siku hizi amebadilika.
KWA NINI ALIKEREKA?
Habari zilizopatikana baadaye zilisema kuwa, Lulu alihamaki kumwona mwandishi huyo aliyeandika habari zake hizo za kula sahani tatu, kwani tangu kutoka kwa stori hiyo amekuwa akitaniwa na mastaa wenzake wakimwambia ‘yeye ni mbaya sana kwenye mechi za ugenini’.
Tafsiri hiyo ni kwamba, Lulu amekuwa akila kupitia kiasi kwenye ‘minuso’ (minuso ni vyakula vya bure kwenye shughuli).

AJITENGA NA BONGO MOVIE
Wakati huohuo, Imelda Mtema anaripoti kuwa, baada ya kufika ndani ya nyumba ya akina Wema, Lulu alionekana kutotaka kujihusisha na baadhi ya wasanii wenzake wa Klabu ya Bongo Movie Unity ambapo alijitenga.

Lulu alijitenga kwa kukaa na mama yake mzazi, Lucresia Karugila na mama mzazi wa marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa.
Wasanii wa Bongo Movie waliokuwepo ambao hawakupata nafasi ya kupiga stori na Lulu kama zamani ni Jacqueline Wolper, Yobnesh Yusuf ‘Batuli’, Jennifer Kyaka ‘Odama’,  Rachel Haule, Kajala Masanja na Eshe Buheti.   

Baadhi ya waombolezaji waliokuwemo walinong’ona kuhusu kitendo cha staa huyo kujitenga wakidai kweli sasa amekua.
 “Mh! Lulu sasa amekua jamani, naona hataki kabisa ushoga na watu, alipofika akasalimia na kwenda kukaa na wazazi wake, ni maajabu,” alisikika akisema mmoja wa waombolezaji ambaye jina lake halikufahamika.

Mwombolezaji mwingine alisikika akisema kuwa mabadiliko yote yanayoonekana kwa Lulu kwa sasa ni kazi ya mama Kanumba.
TUJIKUMBUSHE
Mzee Isaac Sepetu alifariki dunia Oktoba 28, 2013 katika Hospitali ya TMJ, Dar alikokuwa amelazwa kwa matatizo ya kisukari.

MAZISHI YA MZEE SEPETU
Mwili wa marehemu ulitarajiwa kuzikwa jana saa kumi jioni Mjini Zanzibar baada ya kusafirishwa kutoka jijini Dar es Salaam alikofia.
Mungu ailaze pema peponi roho ya marehemu. Amina.

"SIOLEWI NG'O"......LULU

 STAA wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amekataa kabisa suala la kuolewa kwa sasa akidai moyo wake haupo tayari kwa tendo hilo.
 
Lulu alifunguka hayo Jumatatu iliyopita katika kipindi cha Mkasi kinachorushwa kupitia Runinga ya East Africa ambacho humpa nafasi staa kuzungumzia mambo mbalimbali yanayohusu maisha yake na sanaa kwa jumla.
Wakati mahojiano hayo yakiendelea, mmoja wa watangazaji wa kipindi hicho anayefahamika kwa jina la Muba, alimtupia Lulu swali ambalo lilimtaka aeleze utayari wake endapo mtu akijitokeza na kutaka kumuoa.
Sitaki kuolewa kwa sasa, muda wa kuolewa haujafikia. Ukifika nitafanya hivyo lakini kwa sasa sipo tayari kuolewa,” alisema Lulu.
Aidha, Lulu alikiri kuwa licha ya kutokuwa tayari kuolewa lakini amekuwa akipata usumbufu mkubwa wa kutongozwa na wanaume. Aliainisha kuwa alikuwa akitongozwa kabla na baada ya kutoka Segerea alipokuwa akishikiliwa kwa kesi ya kifo cha aliyekuwa mpenzi wake, marehemu Steven Kanumba.


“Watu wananitongoza sana, walikuwa wakifanya hivyo kabla hata sijaingia China (gerezani Segerea) na wameendelea kufanya hivyo hata baada ya kutoka,” alisema Lulu na kuongeza:
Siwezi kuwakubalia sababu sipo tayari kuolewa kwa sasa…muda wa kufanya hivyo haujafika.”
Kuhusu suala la kudaiwa kutembea na bosi wa Kampuni ya Proin Promotion ambayo inamsimamia kisanii kwa sasa, Lulu aliruka viunzi na kudai taasisi hiyo inamlea kama mtoto wa familia na siyo vinginevyo.
Alisema hata madai yanayoelekezwa kwake kuwa Proin wamempa gari na nyumba kama sehemu ya kuhongwa na bosi wa kampuni hiyo, hayana ukweli wowote kwani yeye anafanya kazi kama msanii chini ya kampuni hiyo na hakuna kitu cha ziada.
Hahahaha! Salama (mtangazaji) acha mambo yako bwana… mimi nipo chini ya Proin kwa sasa kwa kipindi flani ambacho nimesaini nao mkataba. Wananilea kama msanii wao, hakuna cha ziada,” alisema Lulu.
Akiendelea kubwabwaja maneno ndani ya kipindi hicho, Lulu aliweka wazi kuwa alikuwa akishindwa kuanika penzi lake na marehemu Kanumba kwa kuwa muda muafaka ulikuwa haujafika na kudai waliishi kama mtu na baba yake kabla hawajawa wapenzi, wakawa wapenzi na mauti yakamkuta Kanumba kabla hawajalianika penzi lao
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. BONGONEWS TZ - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger