Showing posts with label WAASI. Show all posts
Showing posts with label WAASI. Show all posts

HUU NDIO WASIFU WA KAMANDA MKUU WA WAASI WA M-23 KANALI MAKENGA....USOME HAPA...!!

 

Kanali Makenga alizoea kutembea na bakora, ishara kuwa alikuwa mfugaji na pia kamanda wa kijeshi aliyetaka majeshi yake kuwa na nidhamu na kumtii. 

Mrefu na mwembamba , Makenga alikulia katika maeneo ya milimani mkoani Kivu Kusini ndani ya Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo, na alisifika sana kwa kuwa mlenga shabaha na mtu mwenye maarifa na mwenye ujuzi wa kupanga mambo ya kijeshi.

 

Alipata ujuzi wake wa kijeshi nchini Rwanda, ambako alikuwa mmoja wa wapiganaji wa Rais Paul Kagame kabla ya kuchukua mamlaka mjini Kigali.

Baadaye alirejea DR Congo na kuwa mtu mashuhuri katika harakati za kudai haki za wenyeji wa Tutsi wa Congo ambao pia ni wachache.

Maisha ya Kanali Makenga kama mwanajeshi yalifana sana wakati wanajeshi wa M23 walipoteka mji wa Goma , Mashariki mwa DR Congo.

Pia alimshinda hasimu wake wa kijeshi ndani ya M23 Kanali Bosco Ntaganda – na kumwondoa kama kamanda wa wapiganaji wa M23.

Ntaganda alikimbilia nchini Rwanda ambako alijisalimisha kwa ubalozi wa Marekani.

Sasa yuko katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu, ICC, akisubiri kufunguliwa mashitaka ya uhalifu wa kivita.

Ikiwa hatafanikiwa kukubaliana na serikali ya DRC, Makenga huenda na yeye pia akafikishwa ICC.

Ingawa hakuna kibali cha kumkamata, baraza la usalama la Umoja wa Mataifa lilimwekea vikwazo vya usafiri pamoja na kupiga tanji mali zake, mwaka jana likimtuhumu kwa kuongoza uasi wa M23 na kuwafanyia ukatili raia wa Congo, Mashariki mwa nchi.

Lakini kulingana na kanali Makenga, alipigana vita halali akitetea haki za jamii ya watutsi.

Mwaka huu wote kumekuwa na tetesi kua yuko katika hili mbaya ya kiafya na kujisalimisha kwake ni ishara kuwa huenda asirejee tena vitani.


AL SHABAAB TENA!!!: 'WAKIRI KUHISIKA KULIPUA HOTELI....WATU 6 WAUWAWA....SOMA ZAIDI



Wapiganaji wa Kiislam wa Al Shabaab nchini Somalia

Wapiganaji wa Kiislamu wa Al Shabaab nchini Somali wamesema wao ndio waliotekeleza shambulizi la bomu la kujitoa muhanga nje ya hoteli katika mji mkuu wa Mogadishu nchini Somalia ambapo watu sita waliuawa wakiwemo maafisa wa polisi.

Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud amelaani shambulio hilo lilitokea nje ya Hotel ya Maka al Mukurama huku akisisitiza kuwa shambulio halitarudisha nyuma jihada kubwa zinazoendelea za kuleta amani na usalama nchini humo.

Kundi hilo la Al Shabaab ambalo lilifurushwa na majeshi ya Somalia yakishirikiana na yale ya Umoja wa Mataifa AMISOM miaka miwili iliyopita wameapa kuendeleza harakati zao za kufanya mashambulizi.

Hapo awali Waziri wa Mambo ya ndani wa Somalia Abdikarim Hussein Guled aliiambia BBC kuwa watu sita waliuawa na wengine 15 kujeruhiwa katika shambulio hilo la kujitoa muhanga.

Mwandishi wa BBC Ibrahim Mohamed Adan ambaye yupo Mogadishu amesema sauti ya mlipuko ulisikika katikati ya mji huo wa Mogadishu.

-BBC

WAASI WA M23 WAAMUA KUSALITI AMRI MARA BAADA YA KUELEMEWA HUKO MASHARIKI YA CONGO..!!

Wanajeshi wa serikali katika Jmauhuri ya kidemokrasi ya Congo, wanashambulia ngome ya mwisho ya waasi wa M23 katika maeneo ya milimani ,msituni Mashariki mwa nchi.
Mamia ya wakimbizi wanatoroka vita karibu na mpaka wa Mashariki mwa Congo na kuingia nchini Uganda.


















Viongozi wa kundi hilo la M23 walitoa wito kwa wapiganaji wao kusitisha vita na kuruhusu mazungumzo ya amani na serikali.
Kiongozi wa wapiganaji hao Mashariki mwa nchi ametangaza kuwa watasitisha mapigano katika vita vyao na jeshi la serikali.
Bertrand Bisimwa alisema kwenye taarifa kwamba anawasihi wapiganaji wote haraka waache uhasama na wanajeshi, ili kuwezesha mazungumzo ya amani kuendelea.
Wanajeshi wa serikali, wakisaidiwa na kikosi cha kuweka amani cha Umoja wa Mataifa, hivi karibuni wamewasukuma nyuma wapiganaji na kuwatoa katika ngome zao nchini.
Mazungumzo ya amani yanafanywa mjini Kampala, Uganda.

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. BONGONEWS TZ - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger