Home » » MFAHAMU MODEL NA MREMBO KUTOKA TANZANIA ALIYEPAMBA KATIKA COVER YA MAGAZINE KUBWA ZAIDI NCHINI KENYA..!!

MFAHAMU MODEL NA MREMBO KUTOKA TANZANIA ALIYEPAMBA KATIKA COVER YA MAGAZINE KUBWA ZAIDI NCHINI KENYA..!!

Hamisa Hassani Mobeto amezaliwa mwaka 1994 mkoani Mwanza na kabila lake ni Mnyamwezi. Mwanzo wake katika tasnia ya u-miss na modelling ilianza baada ya hamisa kuibuka mshindi wa shindano la  Miss XXL BACK TO SCHOOL BASH  Mwaka 2010 iliyoandaliwa na kipindi cha XXL kutoka Clouds Fm. Mwaka 2011 Hamisa alishiriki mashindano ya Miss Dar Indian Ocean na alifanikiwa kushika nafasi ya pili , pia mwaka huohuo alikua mshindi wa pili wa miss kinondoni na kufanikiwa kuingia kwenye Nusu fainali ya miss Tanzania.
hamisa mobeto bb
Mwaka 2012 hamisa alishiriki kwenye mashindano ya Miss Univeristy Afrika na kuingia hatua ya 10 bora.
hamisa 1
Kutokea Hapo hamisa amekuwa gumzo kwenye tasnia ya uanamitindo na filamu pia. Pia amisa ni video vixen na wengi mnaweza kumuona kwenye video ya Quick Rocka ya My Baby.
hamisa my baby
Mwaka 2014 umeanza vizuri kwa Hamisa baada ya kuweza kutokea kwenye cover page la Pulse Magazine la Nchini Kenya. Akiwa Ndio kwanza ana miaka 21 Hamisa ni mtu wa kuangaliwa sana huu mwaka sababu anategemewa kufanya mambo makubwa zaidi.


hamisa Cover

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. BONGONEWS TZ - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger