Rais Jakaya Kikwete amelihutubia Bunge mjini Dodoma na kueleza kuwa Serikali ya Tanzania haiko tayari kujitoa katika Jumuiya ya Afrika ya Mashariki.
Rais Kikwete alibainisha kwamba kumekuwa na vikao 
visivyo rasmi vinavyofanywa na baadhi ya viongozi wakuu wa Kenya, Uganda
 na Rwanda ambavyo vimekuwa vikipitisha mambo yao bila kushirikisha nchi
 nyingine ndani ya Jumuiya ambazo ni Tanzania na Burundi.
  
“Wenzetu wameshafanya vikao vitatu na kupitisha 
maamuzi manane ya kushirikiana, kwetu sisi tunadhani hizi ni fujo za 
kutaka kuhatarisha uhai wa maisha ya jumuiya yetu ya Afrika Mashariki," 
alisema Rais Kikwete.
  
Alisema Tanzania itaendelea kuheshimu mambo 
yaliyomo kwenye makubaliano ya uanzishwaji wa jumuiya hiyo ambayo ni 
umoja wa forodha, soko la pamoja, sarafu ya pamoja na shirikisho la 
kisiasa bila kukiuka mlolongo wa utekelezaji wake.
  
Mbali na suala la Jumuiya ya Afrika Mashariki, pia
 Rais Kikwete alizungumzia suala la wanajeshi waliokwenda nchini Congo 
DRC kulinda amani, Operesheni Tokomeza dhidi ya ujangili na mchakato wa 
Katiba Mpya
Hotuba nzima itawekwa muda si mrefu
Hotuba nzima itawekwa muda si mrefu
