BIBI Mariam Mponzi (80) amepambana kwa hali na mali kuwatetea wajukuu zake waliotelekezwa na baba yao Emmanuel Yuta.
Emmanuel alidaiwa kuuza nyumba waliyokuwa wakiishi katika Kijiji cha Hatwelo, Kata ya Ijombe, Mbeya Vijijini na kutokomea kusikojulikana huku akiwaacha watoto wake wawili wenye umri wa miaka 9 na 11 wakikosa pa kuishi.
Emmanuel alidaiwa kuuza nyumba waliyokuwa wakiishi katika Kijiji cha Hatwelo, Kata ya Ijombe, Mbeya Vijijini na kutokomea kusikojulikana huku akiwaacha watoto wake wawili wenye umri wa miaka 9 na 11 wakikosa pa kuishi.
Kikongwe huyo 
alichukua hatua hiyo baada ya kubaini kuwa kitendo kilichofanywa na 
mwanaye kwa kushirikiana na serikali ya kijiji si cha kiungwana.
Bibi huyo 
alilazimika kukopa shilingi laki nne kutoka kwa mtu ambaye hakumtaja 
jina kwa lengo la kuzirejesha kwa mtu aliyenunua nyumba hiyo aitwaye 
Dati Nsagaje ambaye alisema akirudishiwa fedha zake angeiachia nyumba 
hiyo.
Akizungumza 
baada ya kurejeshewa nyumba hiyo, kikongwe huyo alisema kwa sasa makazi 
hayo ni mali ya wajukuu zake hivyo mwanae akishindwa kuendelea na maisha
 huko alikokimbilia na kuamua kurejea akatafute sehemu nyingine ya 
kuishi.
Baadhi ya majirani wa eneo hilo walisema kitendo alichokifanya baba wa watoto hao hakipaswi kufumbiwa macho na mlalamikiwa akikamatwa achukuliwe hatua kali za kisheria
Baadhi ya majirani wa eneo hilo walisema kitendo alichokifanya baba wa watoto hao hakipaswi kufumbiwa macho na mlalamikiwa akikamatwa achukuliwe hatua kali za kisheria
 
 
 
 
 
 
 
