Home » » HATIMAYE ABDU KIBA AELEZA CHANZAO CHA UKIMYA WA KAKA YAKE "ALI KIBA"

HATIMAYE ABDU KIBA AELEZA CHANZAO CHA UKIMYA WA KAKA YAKE "ALI KIBA"

 
Ali Kiba, mwimbaji aliyewahi hutajwa na mfalme wa R&B duniani Robert Kelly kama mmoja kati wa wasanii wenye sauti poa zaidi katika mradi wa One 8 amekuwa kimya kwa kipindi cha mwaka mmoja, huku wengi wakitoa sababu kadhaa za kufikirika kuhusu ukimya wake.
Tovuti ya Times Fm imeongea na ndugu wa damu wa Ali Kiba, Abul Kiba ambaye mbali na kuwa msanii aliyetambulishwa kwenye game na kaka yake, amekuwa akisaidia kuzifuatilia na kuzisimamia kazi zake.
Abdu Kiba ameeleza kuwa ukimya wa ndugu yake unatokana na kubanwa na majukumu ya kifamilia.
“Unajua watu wengi wanahisi vibaya sana, mara mwingine anaibuka na kusema amefulia kwenye game,sio kweli naomba niweke sawa kuhusu suala hili ni kwamba Ally Kiba alikuwa na majukumu ya kifamilia pamoja na kazi zake,maana nakumbuka tangu anitambulishe kwenye muziki wa Bongo Flava ndio alianza kubanwa na mambo  yake binafsi.” Amesema Abdu Kiba.
Hata hivyo, mashabiki wa Ali Kiba wana kila sababu ya kukaa mkao wa kusikia hits za mkali huyo mwaka huu.
“Niliwahi kuzungumza nae hivi karibuni, akaniambia mwaka huu anatarajia kuja kivingine katika game. Kwa sasa anajaribu kumalizia baadhi ya nyimbo alizorekodi ili mwaka huu mashabiki wazisikie katika vituo mbalimbali vya radio.” Abdu Kiba aliieleza

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. BONGONEWS TZ - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger