Home » » BAADA YA KUTANGAZA KURUDI SHULE,CHEKA AANZA UTORO SHULENI!

BAADA YA KUTANGAZA KURUDI SHULE,CHEKA AANZA UTORO SHULENI!

Bondia Francis ‘SMG’ Cheka, amedaiwa kuingia darasani siku moja tu tangu aliposajiliwa kama mwanafunzi mpya wa Chuo cha St Joseph cha mjini Morogoro Septemba mwaka jana.
Akizungumza na MWANANCHI, mwalimu wa Cheka aitwaye Mkisi amesema Cheka ameomba kuendelea na masomo baada ya kutoonekana darasani kwa miezi kadhaa bila taarifa yoyote, na kubainisha kuwa hawawezi kumruhusu kuingia muhula wa pili.
Cheka alipewa ufadhili wa masomo chuoni hapo mwaka jana mara baada ya kutwaa ubingwa wa dunia wa WBF Agosti 30, baada ya kumpiga Phil Williams wa Marekani katika pambano lililofanyika jijini Dar es Salaam.
Mkisi amesema kuwa bondia huyo amekosa vipindi kwa muda mrefu hivyo hawezi kuingia muhula mwingine, kwakuwa atakosa vitu vingi hivyo anapaswa kujisajili kama mwanafunzi wa muhula mpya utakaoanza Machi 24.
“Cheka aliingia darasani siku moja na ‘kupotea’ hata hivyo hivi karibuni alikuja na kutuambia anataka kuendelea na shule ingawa hatuwezi kumuendelezea programu yake ya awali,” alisema Mkisi.
-Mwananchi
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. BONGONEWS TZ - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger