Home » » Taarifa muhimu kuhusu kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa kujitolea- 2014

Taarifa muhimu kuhusu kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa kujitolea- 2014


Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) litaandiksiha vijana wa kujiunga na JKT kwa kujitolea kuanzia Januari 2014.

Nafasi hizo zimetolewa kwa Tanzania Bara na Visiwani.
Usaili utaanzia ngazi za Wialaya hadi Mkoa. Vijana wanaopenda kujiunga na JKT kwa kujitolea kwa kipindi cha miaka miwili wapelekea maombi yao kwenye Wilaya waliko.

Mafunzo yataanza mwezi Machi kwa watakaochaguliwa.
Sifa na masharati kwa mwombaji:-
  1. Awe raia wa Tanzania.

  2. Awe na umri wa miaka 18 hadi 23.

  3. Awe na elimu ya darasa la saba hadi kidato cha sita.

  4. Asiwe ameoa, kuolewa na asiwe na mtu anayemtegemea.

  5. Awe tayari kurudi nyumbani baada ya kumaliza mkataba wake na Jeshi la Kujenga Taifa.

  6. Awe na tabia na mwenendo mzuri.

  7. Awe tayari kufuata sheria zote  za Kijeshi zitakazokuwa juu yake wakati akiwa Jeshini (kutoroka, wizi, ulevi, uvutaji bangi, madawa ya kulevya , upatikanaji wa mimba n,k) Jeshini ni makosa makubwa na utaweza kushitakiwa na kusitishiwa mkataba wako na Jeshi la Kujenga Taifa.

TANGAZO HILI LIMETOLEWA NA MAKAO MAKUU YA JESHI LA KUJENGA TAIFA.

>>Via  Wavuti.com
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. BONGONEWS TZ - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger