Home » , » Picha: Sherehe za miaka 50 ya mapinduzi ya Zanzibar...

Picha: Sherehe za miaka 50 ya mapinduzi ya Zanzibar...


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Ali Mohamed Shein akikagua gwaride la heshima wakati wa kilele cha sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar katika Uwanja wa Amani Abeid Karume leo Januari 12, 2014.
Vijana wakiachia njiwa kama alama ya amani wakati wa kilele cha sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar katika Uwanja wa Amani Abeid Karume leo Januari 12, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Ali Mohamed Shein wakimpongeza Rais Yoweri Kaguta Museveni aliyeongea machache wakati wa kilele cha sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar katika Uwanja wa Amani Abeid Karume leo Januari 12, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Ali Mohamed Shein kwa hotuba nzuri aliyotoa  wakati wa kilele cha sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar katika Uwanja wa Amani Abeid Karume leo Januari 12, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Yoweri Kaguta Museveni wakiongea  wakati wa kilele cha sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar katika Uwanja wa Amani Abeid Karume leo Januari 12, 2014.

(PICHA NA IKULU)
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. BONGONEWS TZ - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger