
Tazama video ya magoli ya Simba vs Kagera sugar na fujo zilizotokea uwanjani..

Kocha wa Kagera Sugar amesifia maamuzi ya refa na kusema ‘nafurahi timu imesawazisha kwenye dakika za mwisho na refa amefanya kazi yake kwa sababu ni siku nyingi sana marefa hawagawi penat kama hizo, timu nzuri inacheza mpaka goli’
Kocha Kibaden wa Simba kasema ‘nashukuru tumemaliza mpira salama na vijana wametoka salama, sijafurahishwa na jinsi mpira ulivyochezeshwa, sitaki kusema hayo kwa sababu watu wana macho na wanaweza kukosoa lakini uamuzi haukuwa sawasawa, kama tutaendelea na mpira wa aina hii nafikiri tutaondoka kwenye mwelekeo… naomba TFF mpya iliyokuja ijaribu kutazama watu wapumbavu wa aina hii wanaokuja pale kuwaudhi watu, sijafurahishwa na mpira ulivyochezeshwa mwanzo hadi mwisho na nilijua kitatokea nini’
NUSU UTUPU YA LINAH YAWADATISHA WANAUME..!
![]() |
Linah akiwa jukwaani wakati wa shoo ya Fiesta 2013 jijini Dar. |
Mavazi ya nusu utupu ambayo msanii Esterlina Sanga ‘Linah’ hupenda kuyavaa hasa kwenye matamasha yamekuwa yakiwadatisha wanaume na wengine kuomba kupiga naye picha kwa lengo la ‘kujipoza’ kama ilivyotokea kwenye Fiesta, Dar hivi karibuni.


Linah akipozi na baadhi ya wanaume walioomba kupiga naye picha.
Ijumaa limekuwa likimfuatilia Linah na kubaini kuwa kila mara hupenda kuvaa nguo zinazoacha wazi mapaja na kitovu chake na watu ambao amekuwa akipiga nao picha ni wanaume ambao wengi huonekana wakiwa wamemshika kimahaba.

GPL
PAMOJA NA MISHAHARA YAO WABUNGE ....! JE NI HALALI KWAO KULALAMIKA MASLAHI MADOGO..??

Imethibitika rasmi kuwa wakati wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano ya Tanzania wakilalamikia maslahi madogo, mbunge mmoja hulipwa mshahara wa Sh. milioni 11 kwa mwezi.
Kiasi hiki hakijumuishi posho ya Sh. 330,000 anayolipwa mbunge kwa kuhudhuria kikao kimoja kwa siku. Posho ni Sh. 80,000 za kujikimu akiwa nje ya jimbo lake, posho ya vikao Sh. 200,000 kwa siku na mafuta ya gari Sh. 50,000, jumla kuwa Sh. 330,000 kwa siku.
Aidha, mbunge mmoja hulipwa ‘gratuity’ (kiinua mgongo au bahashishi) ya Sh. milioni 72 baada ya kumaliza kipindi chake cha miaka mitano cha ubunge.
Aidha, wabunge hupewa fedha za Mfuko wa Jimbo Sh. milioni 30 kila mwaka kwa ajili ya kusaidia shughuli za maendeleo katika majimbo yao.
TAZAMA VIWANGO VIPYA VYA ALAMA ZA UFAULU WA ELIMU YA SEKONDARI..SOMA HAPA...!
UPANGAJI WA VIWANGO VYA ALAMA, MATUMIZI YA ALAMA ENDELEVU YA MWANAFUNZI NA UFAULU
UTANGULIZI
Wizara imekusanya maoni ya Wadau wa Elimu kuhusu Upangaji wa Viwango vya Alama (Grade Ranges) katika Mitihani ya Kuhitimu Kidato cha Nne na cha Sita pamoja na Matumizi ya Alama za Tathmini Endelevu ya Mwanafunzi (Continuous Assessment ama CA) kwa ajili ya kuamua kiwango cha ufaulu wa mwanafunzi.
Maoni ya wadau yamekusanywa kwa sababu kwa muda mrefu sasa upangaji wa viwango vya alama vinavyotumika na utaratibu wake katika mitihani ya kuhitimu Kidato cha Nne na Kidato cha Sita umekuwa haufanani pamoja na kwamba mitihani hiyo yote ni ya elimu ya sekondari.
Pia mfumo masuala mbalimbali ya mitihani katika elimu ya sekondari umekuwa na miundo tofauti ikiwemo ule unaotumika shuleni na ule wa Baraza la Mitihani la Taifa. Kwa sasa kuna miundo mikuu miwili katika mfumo huo.
Muundo wa Kwanza ni upangaji wa viwango katika ngazi ya Shule ambapo Alama Mgando (Fixed Grade Ranges) zifuatazo hutumika kupanga madaraja: A = 81 – 100; B = 61 – 80; C = 41 – 60; D = 21 – 40 na F = 0 – 20. Muundo huu umetumika kwa muda mrefu na umezoeleka kwa walimu na wanafunzi wa elimu ya sekondari kwa ujumla.
Muundo wa Pili ni wa viwango vinavyotumiwa na Baraza la Mitihani la Taifa ambapo ambapo kabla ya mwaka 2012 muundo wa viwango nyumbufu (flexible grade ranges) ulitumika.
Katika muundo huu uwigo wa alama ulibadilika badilika kulingana na hali ya matokeo ilivyokuwa kwa mwaka husika. Lakini kuanzia mwaka 2012, Serikali iliamua kutumia mfumo wa Upangaji wa Alama Mgando (Fixed Grade Range) kwa Kidato cha Nne na Kidato cha Sita.
Katika mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2012 Baraza lilitumia mfumo huu wa alama mgando ambapo: A = 80 – 100, B = 65 – 79, C = 50 – 64, D = 35 – 49, F = 0 – 34.
Kwa upande wa Kidato cha Sita Baraza lilitumia mfumo wa A = 80 – 100; B = 75 - 79; C = 65 – 74; D = 55 – 64; E = 45 – 54; S = 40 – 44 na F = 0 – 39.
Mifumo hii ya Baraza haikuwa inafahamika kwa wadau na hivyo kuwa sehemu ya malalamiko katika sekta ya elimu na mafunzo.
Vilevile, Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 1995 imeelekeza kwamba katika kuamua kiwango cha ufaulu wa mwanafunzi wa elimu ya sekondari, Alama za CA zitachangia asilimia hamsini (50%) na Mtihani wa mwisho utachangia asilimia hamsini (50%).
Kwa upande wa Zanzibar, CA zimekuwa zikiandaliwa kwa mfumo wa asilimia arobaini (40%) na mtihani wa mwisho asilimia sitini (60%). Pamoja na kwamba Baraza halijawahi kuutumia mifumo hii tangu ilipowekwa, kumekuwa na mitazamo, maoni na mapendekezo tofauti katika muundo na matumizi ya alama za CA.
Kuna mawazo pia kwamba mfumo wa CA kuchangia matokeo ya mwisho ya mwanafunzi pia utumike kwa watahiniwa wa kujitegemea (private candidates).
Kwa sasa matokeo ya mitihani ya watahiniwa hawa yamekuwa yakitumia alama za mtihani wa mwisho tu na hivyo kutafsiriwa kama utaratibu ambao unamwonea mwanafunzi ambaye anahamu ya kujiendeleza kielimu lakini anakwama kwa sababu mfumo unaotumika siyo rafiki kwa mtahiniwa.
Kwa mantiki hii, Wizara imedhamiria kufanya harmonization ya masuala ya alama katika mitihani ya Kidato cha Nne na Kidato cha Sita ili kupata muundo mmoja na ulio wazi kwa wadau wote wa elimu ya sekondari.
Lakini pia serikali imedhamiria kuhakikisha tathmini za wanafunzi katika ngazi mbalimbali zinakwenda sambamba na matarajio ya mitaala inayotumika na ambayo inahuishwa mara kwa mara ili iendane na wakati na mahitaji ya elimu katika ngazi mbalimbali.
VIWANGO NA UTARATIBU KUANZIA MWAKA 2013 KWA KIDATO CHA NNE NA KIDATO CHA SITA KWA MWAKA 2014
Baada ya kufanya tathmini ya maoni mbalimbali ya wadau, misingi ifuatayo ilizingatiwa katika maamuzi kuhusu makundi ya alama na muachano wake:
a) Alama zitakazotumika zitakuwa A, B, C, D, E na F. Muachano wa alama kati ya kundi moja hadi jingine utafanana, isipokuwa tu pale ambapo itaonekana kuna sababu na hakuna athari za kuwa na muachano tofauti na ule ambao umetumika katika makundi mengine.
b) Makundi ya alama hayatakuwa na clusters isipokuwa pale ambapo itaonekana kufanya hivyo kunaleta tija katika kupata picha ya wahitimu kwa ajili ya matumizi mbalimbali. Kwa mantiki hii
(i) makundi ya alama A, C, D, E na F yabaki na cluster moja moja bali kundi la alama B litakuwa na clusters mbili. Kundi la kwanza litakuwa la wale ambao wamepata alama kati ya 50 mpaka 59 na litaitwa B na lingine litakuwa la wale ambao wamevuka uwigo wa 50 hadi 59 na kuelekea uwigo wa 60 hadi 74 na hili litaitwa B+ (angalia jedwali hapo chini).
(ii) Pamoja na kuwa na muachano wa alama 26 kama jedwali linavyoonesha hapo chini, alama A kwa miaka mingi imekuwa ikianzia alama 75 hadi 100 na kwamba pamoja na uwigo huo bado wanaofaulu kwa kiwango hicho ni wachache sana.
Kwa mantiki hii, hakuna haja ya kubadilisha uwigo ila juhudi ziendelee katika ufundishaji na ujifunzaji ili kiwango cha ufaulu kiongezeke na kupata wanafunzi wengi zaidi wanaofaulu katika kundi hili.
(iii) Pia, pamoja na kuwa na muachano wa alama 20 kama jedwali linavyoonesha hapo chini kwa miaka mingi, huko shuleni mwanafunzi aliyepata alama 21 na hadi 30 alihesabiwa kuwa na ufaulu wa chini kabisa au hafifu kwa kiwango cha alama D na ingawa ilikubalika ufaulu wa aina hiyo kwa mazingira ya nchi yetu unaridhisha.
Alama Filikuwa ni kwa wale waliopata chini ya hapo. Hivyo, alama F itaendelea kuwepo na itaanzia alama 0 hadi 19 na E itaanzia alama 20 hadi 29 na D – 30 -39.
Lengo la muundo huu ni kuwa alama mbalimbali, isipokuwa kwa makundi machache, zianzie kwenye 0 yaani 0, 10, 20, 30, 40 na kuendelea badala ya kuanzia kwenye moja yaani 1, 11, 21, 31, 41 na kuendelea.
Hii ni kwa ajili ya kuleta mtizamo unaofanana katika ngazi mbalimbali za elimu ambapo kwa sasa ngazi ambazo siyo za elimu msingi na sekondari zinatumia muundo wa kuanzia kwenye 0 badala ya 1.
c) Uwigo wa jumla wa alama kwa Kidato cha Nne na Kidato cha Sita utaendelea kuwa wa alama 0 hadi 100 na kila kundi katika uwigo huu limepewa tafsiri kwa ajili ya kuamua mambo mbalimbali yanayohusu maendeleo ya mwanafunzi kulingana na malengo ya mtihani husika. Kimsingi, tafsiri zifuatazo zitakatumika
(i) Alama A itakuwa na maana ya ufaulu uliojipambanua (distincion or outstanding performance),
(ii) Alama B+ itakuwa na maana ya ufaulu bora sana (excellent performance),
(iii) Alama B itakuwa na maana ya ufaulu mzuri sana ( very good perfomance),
(iv) Alama C itakuwa na maana ya ufaulu mzuri (good performance);
(v) Alama D itakuwa na maana ya ufaulu wa wastani (low performance),
(vi) Alama E itakuwa na maana ya ufaulu hafifu (very low performance), na
(vii) Alama F itakuwa na maana ya ufaulu usioridhisha (unsatisfactory performance).
Wataalamu katika maeneo mbalimbali ya elimu na ulimwengu wa kazi, kwa kushirikiana na Wizara, watatoa maana ya tafsiri hizi kiutendaji katika maeneo yao kulingana pia na mahitaji yao.
d) Alama C iwe ndiyo alama ya ufaulu mzuri ambao hauhitaji urekebu wa lazima, wakati alama D na E ni alama za ufaulu unaohitaji urekebu kadri mwanafunzi atakavyokuwa anaendelea na masomo ili kuthibitisha kama mlengwa anaweza na kulingana na mahitaji ya eneo husika (targeted remediation).
Alama F iwe alama ya eneo linalohitaji urekebu wa hali ya juu (intesive remediation) ili mwanafunzi huyo aweze kumudu masomo kadri anavyoendelea kukua kielimu ama atakapoingia katika ulimwengu wa kazi.
e) Makundi ya alama yatajumuisha CA kwa kiwango cha asilimia isiyozidi 40 na mtihani wa mwisho kwa asilimia isiyozidi 60 kwa makundi yote ya watahiniwa ikiwemo wale wa kujitegemea (private candidates).
Hii ni kwa kuzingatia kwamba CA siyo vizuri izidi uwigo wa alama ya ufaulu mzuri unapoanzia ambayo ni C au 40.
f) CA kwa upande wa Kidato cha Nne zitokane na mtihani wa Kidato cha Pili (alama 15), matokeo ya Kidato cha Tatu (alama 5 kwa kila muhula, na hivyo jumla ya alama 10), mtihani wa Mock (alama 10) na kazi mradi au Projects (alama 5).
Kwa upande wa Kidato cha Sita, CA iendelee kutokana na muundo unaotumika sasa.
g) CA zitumike pia kwa watahiniwa wa kujitegemea. Kwa upande wa watahiniwa wa kujitegmea ambao wanarudia Mitihani, CA zao zitumike zile zilizotumika kutoa matokeo yake ya mitihani ya awali.
Kwa watahiniwa wa kujitegemea waliopitia mfumo wa Qualifying Test (QT), matokeo ya QT yatumike kama CA na mtihani wa mwisho uchangie alama 60.
h) Kwa vile alama endelevu kwa mwaka 2013 kwa wanafunzi wa Kidato cha Nne tayari zimeshawasilishwa Baraza la Mitihani Tanzania, alama hizo zichangie asilimia 40 katika mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2013.
i) Muundo wa wastani wa alama katika ufaulu (Grade Points Average ama GPA) utaandaliwa na kuanza kutumika pale utakapokuwa tayari na wadau wataelimishwa kuhusu muundo huo ili wapate kuufahamu na manufaa yake katika elimu ya sekondari.
j) Muundo huu mpya wa alama utatumika kwa mzunguko wa miaka minne kabla haujahuishwa tena ili kuupa muda wa kutosha kuona aina ya changamoto zinazojitokeza na jinsi ya kuzishughulikia.
Aina hii ya muda itaruhusu vidato vinne vya elimu ya sekondari ya kawaida na nane ya elimu ya sekondari ya juu kupimwa.
Hata hivyo, uhusihaji wa masuala ya mitihani unaweza ukafanyika iwapo matokeo ya uhuishaji wa mitaala kwa ujumla utahitaji pia eneo la mitihani liguswe na kuhuishwa pia.
Kwa mantiki hii, viwango vya alama na ufaulu ni kama inavyooneshwa kwenye jedwali la 1 hapa chini:
Jedwali Na 1
MUUNDO WA ALAMA NA UFAULU
ALAMA | UWIGO WA ALAMA | IDADI YA ALAMA | TAFSIRI |
A | 75 - 100 | 26 | Ufauli Uliojipambanua |
B+ | 60 - 74 | 15 | Ufaulu bora sana |
B | 50- 59 | 10 | Ufaulu mzuri sana |
C | 40 - 49 | 10 | Ufaulu mzuri |
D | 30 - 39 | 10 | Ufaulu Hafifu |
E | 20 - 29 | 10 | Ufaulu hafifu sana |
F | 0 - 19 | 20 | Ufaulu usioridhisha |
Kwa aina hii ya muundo wa alama, na kwa kuwa muundo wa GPA utaanza kuandaliwa na wadau kuelimishwa kabla haujaanza kutumika, katika kipindi hiki mpaka wakati huo, muundo wa madaraja utakuwa kama inavyooneshwa kwenye jedwali la 2 hapa chini.
Jedwali Na 2
MUUNDO WA MADARAJA
MUUNDO WA ZAMANI | MUUNDO MPYA | MAELEZO | ||
POINTI | DARAJA | POINTI | DARAJA | |
7-17 | 1 | 7-17 | I | Kundi la ufaulu uliojipambanua na bora sana |
18-21 | II | 18-24 | II | Kundi la ufaulu mzuri sana |
22-25 | III | 25-31 | III | Kundi la ufaulu mzuri na wa wastani |
26-33 | IV | 32-47 | IV | Kundi ufaulu hafifu |
34-35 | 0 | 48-49 | V | Kundi la ufaulu usioridhisha |
Wataalamu
wa mifumo ya mitihani watalifanyia kazi zaidi jedwali hili la madaraja
ili liweze kutumika kwa ufanisi katika kipindi hiki cha mpito.
Kwa mantiki hii, Daraja Sifuri linafutwa na kuwekwa daraja litakalojulikana kama Daraja la Tano na ambalo litakuwa ndilo la mwisho kabisa katika ufaulu.
HITIMISHO
Mabadiliko haya yamefanyika ili kuendelea kuimarisha mfumo wetu wa elimu na kuweka wazi taratibu mbalimbali kwa ajili ya mitihani na masuala mengine.
Yako
mambo mengi mengine ambayo hayana budi kuendelea kuimarishwa ikiwemo
mfumo wa mitaala, walimu, mazingira ya kujifunzia na kufundishia pamoja
na vitabu na vifaa vingine muhimu katika elimu.
Masuala haya yanaendelea kuangaliwa kupitia mikakati mbalimbali ikiwemo mpango wa Matokeo Makubwa Sasa ama Big Results Now (BRN).
Ushirikiano
wa wadau wote ili kuleta tija kwenye elimu ni muhimu sana na hivyo
wizara itaendelea kuwashirikisha wadau wote kwa kadri itakavyohitajika
na wadau pia wanaombwa wasiache kuishirikisha wizara pale watakapokuwa
na jambo lolote ambalo linahitaji ushirikiano ili kwa pamoja tuweze
kupata mafanikio katika sekta ya elimu.
Imetolewa na,
KATIBU MKUU
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
BINTI AAMUA KUJINYONGA MPAKA KUFA MARA BAADA YA WAZAZI WAKE KUMKATAZA ASITUMIE FACEBOOK NA AZINGATIE MASOMMO ZAIDI...!!
Binti
wa miaka 17 nchini India katika jiji la Parbhani amejiua baada ya
wazazi wake kumkataza asitumia ukurasa wa Facebook ili apate muda wa
kuzingatia masomo aliyokuwa akishindwa vibaya darasani tofauti na
ilivyokuwa kabla yajaanza kutumia Facebook ambapo alikuwa akifaulu.
Aishwarya Dahiwal alikutwa ananing'inia chumbani kwake baada ya kuzuka mabishano baina yake na wazazi wake ambao
walikuwa wanakerwa na muda mwingi anaoutumia kwenye mtandao wa Facebook na mazungumzo marefu kwenye simu yake ya mkononi.
Gazeti tando la habari za teknolojia, Gawker limeripoti kuwa marehemu aliacha ujumbe usemao kuwa asingweza kuishi bila mitandao ya kijamii na moja ya yaliyoandikwa humo ni pamoja na kuuliza, "Je, Facebook ni mbaya hivyo?" "Siwezi kuishi katika nyumba yenye vizuizi vya aina hii na siwezi kuishi bila Faceboook" na hivyo kuwalaumu wazazi wake kwa hatua ya kujiua aliyoichukua.
Kama ilivyo kwa wazazi wowote ambao kwa kawaida wameyaona maisha na kufahamu mbinu za kukabiliana nayo, walikuwa na nia njema ya kutaka kumsaidia mtoto wao aweze kufanikiwa lakini mabadiliko ya kila kizazi yanayokuja na changamoto zake ambazo hazina vigezo wala vielelezo vya namna ya kumsaidia mtoto akabiliane navyo vyema hali akiyamudu maisha kwa uwiano, walijikuta katika huzuni ya kulazimika kukubaliana na jambo ambalo hawakutarajia lingetokea.
Bila shaka ujio wa internet umebadili maisha ya vijana na familia kwa ujumla. Pamoja na kuwa na faida nyingi kwa wale wanaojua namna ya kuitumia vyema, bado madhara na hasara zake ni kubwa ambazo zinaonekana dhahiri kwenye mahusiano ya aina zote iwe kikazi, kifamilia, kijamii au hata kutoka kwa mtu msiyefahamiana kabisa ila kwa kuwa amekuona kwenye moja ya mitandao ya kijamii, anaweza kukutisha na hata kukudhuru.
Jirani yangu alinisimulia jinsi rafiki yake alivyoibiwa nyumbani kwake baada ya kuandika kwenye ukurasa wake wa Twitter kuwa baada ya uchovu wa kazi wiki nzima, amekwenda kubarizi ufukweni na atarudi majira ya jioni hivi, kwa kuwa anwani yake ilikuwa kwenye wasifu wake (profile details) basi taarifa hizo zikawa maelezo ya kutosha kwa wezi kufanya watakavyo.
Aishwarya Dahiwal alikutwa ananing'inia chumbani kwake baada ya kuzuka mabishano baina yake na wazazi wake ambao
Gazeti tando la habari za teknolojia, Gawker limeripoti kuwa marehemu aliacha ujumbe usemao kuwa asingweza kuishi bila mitandao ya kijamii na moja ya yaliyoandikwa humo ni pamoja na kuuliza, "Je, Facebook ni mbaya hivyo?" "Siwezi kuishi katika nyumba yenye vizuizi vya aina hii na siwezi kuishi bila Faceboook" na hivyo kuwalaumu wazazi wake kwa hatua ya kujiua aliyoichukua.
Kama ilivyo kwa wazazi wowote ambao kwa kawaida wameyaona maisha na kufahamu mbinu za kukabiliana nayo, walikuwa na nia njema ya kutaka kumsaidia mtoto wao aweze kufanikiwa lakini mabadiliko ya kila kizazi yanayokuja na changamoto zake ambazo hazina vigezo wala vielelezo vya namna ya kumsaidia mtoto akabiliane navyo vyema hali akiyamudu maisha kwa uwiano, walijikuta katika huzuni ya kulazimika kukubaliana na jambo ambalo hawakutarajia lingetokea.
Bila shaka ujio wa internet umebadili maisha ya vijana na familia kwa ujumla. Pamoja na kuwa na faida nyingi kwa wale wanaojua namna ya kuitumia vyema, bado madhara na hasara zake ni kubwa ambazo zinaonekana dhahiri kwenye mahusiano ya aina zote iwe kikazi, kifamilia, kijamii au hata kutoka kwa mtu msiyefahamiana kabisa ila kwa kuwa amekuona kwenye moja ya mitandao ya kijamii, anaweza kukutisha na hata kukudhuru.
Jirani yangu alinisimulia jinsi rafiki yake alivyoibiwa nyumbani kwake baada ya kuandika kwenye ukurasa wake wa Twitter kuwa baada ya uchovu wa kazi wiki nzima, amekwenda kubarizi ufukweni na atarudi majira ya jioni hivi, kwa kuwa anwani yake ilikuwa kwenye wasifu wake (profile details) basi taarifa hizo zikawa maelezo ya kutosha kwa wezi kufanya watakavyo.
JE UNAZIFAHAMU KAULI ZA HATARI KWENYE MAPENZI....!! SOMA HAPA KUZIFAHAMU, USIJE UKAACHWA KWA KAULI ZAKO..
WAKATI fulani
kwenye uhusiano suala la migogoro ni la kawaida. Inaelezwa kwamba,
wapenzi wanapoingia kwenye kuhitilafiana ndiyo uimara wa penzi
unapotokea.

Yeah! Matatizo hukomaza akili. Mkikaa bila kugombana ni vigumu kujua namna mwenzako alivyo hasa kama ikitokea kutoelewana baadaye.
Rafiki zangu, kugombana hakuna maana ya kumalizika kwa uhusiano hasa kwa wale walio kwenye ndoa. Mambo yanatokea, yanatatuliwa na mwisho wake maisha yanaendelea kama kawaida.
Kwa bahati mbaya sana ni kwamba, wengine wanapokuwa kwenye migogoro na wenzi wao, badala ya kutafuta njia za utatuzi, wanazalisha tatizo lingine!
Jambo la kusikitisha ni kuwa, tatizo jipya linalozaliwa linaweza kusababisha matatizo makubwa zaidi katika uhusiano huo na mwisho wake kusababisha kuachana kabisa.
Ngoja tupanue mawazo yetu leo hapa, Zipo kauli ambazo ukizitoa kwa mpenzi/mke/mume wako wakati mkiwa kwenye ugomvi, zinaweza kuzalisha tatizo kubwa zaidi mbeleni.
KWA NINI KAULI?
Inawezekana ukajiuliza; ni kwa nini nimesema kauli? Rafiki zangu, kwa kawaida, watu wakiwa kwenye ugomvi, jambo kubwa linalotokea ni kutupiana maneno.
Katika hali hiyo basi, kwa wenzi au wanandoa ni vyema kuchunga ndimi zao maana zinaweza kusababisha matatizo makubwa siku zijazo. Baadhi ya Kauli hizo na kama zifuatazo hapa chini...
‘HUNA AKILI’
Wako baadhi ya watu wakigombana (hasa wanaume) wamekuwa na tabia ya kuwaambia wanawake wao: “Wewe huna akili kabisa...yaani hutumii akili kabisa katika kufanya mambo yako.
“Unakurupuka tu. Sasa ishu kama hii, hata mtoto mdogo anajua ni makosa, inakuwaje wewe unakosea?”
Hili ni jeraha la moyo. Mwanamke ukimwambia hana akili anajisikia vibaya, unampa kovu kubwa moyoni mwake. Anajiona wa hali ya chini na anahisi ameshuka thamani yake.
Kwake, kumwambia hana akili, ataanza kuwaza kuwa yupo mwanamke mwingine ambaye kwako ana akili kuliko yeye. Ni maumivu makali sana kwake.
‘NITAKUACHA’
Baadhi ya wanaume wana ulemavu huu. Ugomvi kidogo tu, atamwambia mwenzake: “Endelea na tabia zako za hovyo, ipo siku utajuta. Nimevumilia mengi sana lakini kuna siku nitachoka.
“Hutaamini macho yako. Siyo lazima niishi na wewe. Siwezi kuendelea kuteseka nikiwa na wewe. Nitakuacha nakuambia ukweli.”
Hii ni kauli mbaya ambayo inapandikiza chuki ndani ya moyo wa mwanamke. Kwanza kwa kumwambia hivi, hata kama alikuwa hakusaliti, unamfanya aanze kufikiria kutafuta mtu mwingine wa kumliwaza.
Kauli hii hasa kama ukiirudia zaidi ya mara mbili, humkaa akilini mwake na huanza kuwaza kuhusu kuwa na mwanaume mwingine nje ili apate mahali ambapo hata kama ukimuacha, atapata pumziko la uhakika.
‘NAKUVUMILIA TU’
Ni kweli mapenzi ni uvumilivu. Kuvumiliana ni siri ya uhai wa ndoa nyingi lakini hilo linapaswa kubaki moyoni.
Kugombana na mwenzako halafu umwambie kuwa unamvumilia tu, inamaana kwamba kuna siku uvumilivu wako utaondoka na utafanya maamuzi magumu – kuachana!
Si kauli njema kwa mwenzi wako. Mbaya zaidi humfanya aanze kufanya maandalizi ya mtu wa kuziba nafasi yako hata kama ni kwa usaliti.
‘KUNA SIKU UTAJUTA’
Kauli hii haina tofauti kubwa sana na iliyotangulia maana kinachofanyika hapa ni kumuandaa mwenzi wako kwa ajili ya matatizo siku zijazo.
Kumwambia: “Kuna siku utajuta, endelea na mambo yako tu, utaona.” Hii inamaanisha kwamba, uamuzi ulio ndani yako si mzuri kwake lakini ni suala la muda tu.
Ataamini (na ndivyo ilivyo mara nyingi) kuna muda ambao atajuta sana kwa sababu yako.
Hiyo ni sawa na kutengeneza bomu unaloliandaa kulilipua muda ujao.
Hizi ni baadhi ya kauli ambazo ni wapenzi wengi wanapenda kuzitumia wakati wa malumbano, lakini zina madhara makubwa sana katika maisha ya baadae ya mahusiano yenu kwahiyo chunga sana unapogombana na mpenzi wako kauli zakumwambia....

Yeah! Matatizo hukomaza akili. Mkikaa bila kugombana ni vigumu kujua namna mwenzako alivyo hasa kama ikitokea kutoelewana baadaye.
Rafiki zangu, kugombana hakuna maana ya kumalizika kwa uhusiano hasa kwa wale walio kwenye ndoa. Mambo yanatokea, yanatatuliwa na mwisho wake maisha yanaendelea kama kawaida.
Kwa bahati mbaya sana ni kwamba, wengine wanapokuwa kwenye migogoro na wenzi wao, badala ya kutafuta njia za utatuzi, wanazalisha tatizo lingine!
Jambo la kusikitisha ni kuwa, tatizo jipya linalozaliwa linaweza kusababisha matatizo makubwa zaidi katika uhusiano huo na mwisho wake kusababisha kuachana kabisa.
Ngoja tupanue mawazo yetu leo hapa, Zipo kauli ambazo ukizitoa kwa mpenzi/mke/mume wako wakati mkiwa kwenye ugomvi, zinaweza kuzalisha tatizo kubwa zaidi mbeleni.
KWA NINI KAULI?
Inawezekana ukajiuliza; ni kwa nini nimesema kauli? Rafiki zangu, kwa kawaida, watu wakiwa kwenye ugomvi, jambo kubwa linalotokea ni kutupiana maneno.
Katika hali hiyo basi, kwa wenzi au wanandoa ni vyema kuchunga ndimi zao maana zinaweza kusababisha matatizo makubwa siku zijazo. Baadhi ya Kauli hizo na kama zifuatazo hapa chini...
‘HUNA AKILI’
Wako baadhi ya watu wakigombana (hasa wanaume) wamekuwa na tabia ya kuwaambia wanawake wao: “Wewe huna akili kabisa...yaani hutumii akili kabisa katika kufanya mambo yako.
“Unakurupuka tu. Sasa ishu kama hii, hata mtoto mdogo anajua ni makosa, inakuwaje wewe unakosea?”
Hili ni jeraha la moyo. Mwanamke ukimwambia hana akili anajisikia vibaya, unampa kovu kubwa moyoni mwake. Anajiona wa hali ya chini na anahisi ameshuka thamani yake.
Kwake, kumwambia hana akili, ataanza kuwaza kuwa yupo mwanamke mwingine ambaye kwako ana akili kuliko yeye. Ni maumivu makali sana kwake.
‘NITAKUACHA’
Baadhi ya wanaume wana ulemavu huu. Ugomvi kidogo tu, atamwambia mwenzake: “Endelea na tabia zako za hovyo, ipo siku utajuta. Nimevumilia mengi sana lakini kuna siku nitachoka.
“Hutaamini macho yako. Siyo lazima niishi na wewe. Siwezi kuendelea kuteseka nikiwa na wewe. Nitakuacha nakuambia ukweli.”
Hii ni kauli mbaya ambayo inapandikiza chuki ndani ya moyo wa mwanamke. Kwanza kwa kumwambia hivi, hata kama alikuwa hakusaliti, unamfanya aanze kufikiria kutafuta mtu mwingine wa kumliwaza.
Kauli hii hasa kama ukiirudia zaidi ya mara mbili, humkaa akilini mwake na huanza kuwaza kuhusu kuwa na mwanaume mwingine nje ili apate mahali ambapo hata kama ukimuacha, atapata pumziko la uhakika.
‘NAKUVUMILIA TU’
Ni kweli mapenzi ni uvumilivu. Kuvumiliana ni siri ya uhai wa ndoa nyingi lakini hilo linapaswa kubaki moyoni.
Kugombana na mwenzako halafu umwambie kuwa unamvumilia tu, inamaana kwamba kuna siku uvumilivu wako utaondoka na utafanya maamuzi magumu – kuachana!
Si kauli njema kwa mwenzi wako. Mbaya zaidi humfanya aanze kufanya maandalizi ya mtu wa kuziba nafasi yako hata kama ni kwa usaliti.
‘KUNA SIKU UTAJUTA’
Kauli hii haina tofauti kubwa sana na iliyotangulia maana kinachofanyika hapa ni kumuandaa mwenzi wako kwa ajili ya matatizo siku zijazo.
Kumwambia: “Kuna siku utajuta, endelea na mambo yako tu, utaona.” Hii inamaanisha kwamba, uamuzi ulio ndani yako si mzuri kwake lakini ni suala la muda tu.
Ataamini (na ndivyo ilivyo mara nyingi) kuna muda ambao atajuta sana kwa sababu yako.
Hiyo ni sawa na kutengeneza bomu unaloliandaa kulilipua muda ujao.
Hizi ni baadhi ya kauli ambazo ni wapenzi wengi wanapenda kuzitumia wakati wa malumbano, lakini zina madhara makubwa sana katika maisha ya baadae ya mahusiano yenu kwahiyo chunga sana unapogombana na mpenzi wako kauli zakumwambia....
WAPENZI: JE MPENZI WAKO AMEKUSALITI..?? SOMA HAPA KUFAHAMU HATUA KUMI ZA KUCHUKUA BAADA YA KUSALITIWA...
Katika maisha
ya kimapenzi hakuna kitu kinachouma kama kusalitiwa, tena kusalitiwa
kunakouma zaidi ni pale unapobaini mpenzi wako kampa penzi mtu unayemjua
halafu ukijilinganisha wewe na huyo aliyepewa unashindwa kuelewa
kilichomshawishi mpenzi wako.
Lakini licha ya kwamba usaliti si kitu kizuri, watu wamekuwa wakisalitiana, tena sana tu. Inafika wakati unashindwa kuamini kama yupo mtu ambaye hajawahi kumsaliti mpenzi wake.
Niseme tu kwamba wapo wachache waliotulia ila asilimia kubwa ya walio kwenye uhusiano ni wasaliti hata tafiti zimethibitisha hilo. Kama hali yenyewe iko hivyo, cha kujiuliza ni kwamba unapobaini mpenzi wako kakusaliti ni kipi unachotakiwa kufanya? Je, ni kuamua kunywa sumu kama ambavyo wamekuwa wakifanya wengine? Sidhani kama huo ni uamuzi sahihi.
Mtaalam wa masuala ya mapenzi James Johnson kutoka Marekani amependekeza mambo 10 unayoweza kufanya baada ya kubaini kuwa mpenzi wako amekusaliti.
1. Kubaliana na kilichotokea
Kama kishakusaliti ni tukio ambao limeshatokea na haliwezi kufutika. Kubali kuwa umetendwa, huzunika lakini mwisho liache lipite ili uweze kujipanga upya.
2. Usijilaumu
Wapo ambao wakishasalitiwa hujuta kukubali kuingia kwenye uhusiano na watu waliowatenda. Utamsikia mtu akisema ‘najuta kumkubalia awe mpenzi wangu’. Kujilaumu kwa namna hiyo hukutakiwi kwani kutakufanya uzidi kunyong’onyea.
3. Jitoe
Jifanye kama vile aliyesalitiwa siyo wewe bali ni rafiki yako kisha jiulize ungemshaurije? Ushauri ambao ungempata basi uchukue kisha uufanyie kazi.
4. Pima ulivyoathirika
Je, kitendo cha mpenzi wako kukusaliti kimekukosesha imani juu yake? Kama ni hivyo, unadhani una sababu ya kuendelea kuwa naye au unahisi madhara aliyokupatia huwezi kumvumilia?
5. Mpasulie ukweli
Kwa vyovyote utakavyoamua ni lazima umweleze juu namna alivyokuumiza kwa usaliti wake. Hata kama utampa nafasi nyingine lazima ajue jinsi alivyokuumiza ili iwe changamoto kwake.
6. Chunguza kwa nini kakusaliti
Usiliache likapita hivi hivi, unatakiwa kujua sababu ya yeye kukusaliti. Je, kuna ambacho anakikosa kwako au ni tamaa zake tu? Jibu utakalolipata litakusaidia katika maisha yako ya kimapenzi.
7. Usikubali akulainishe
Huenda huyo mpenzi wako ni ‘msanii’ na anaweza kukulainisha kwa maneno ambayo yanaweza kukufanya ukalichukulia tukio hilo kiurahisi. Kuwa na msimamo na eleza hisia zako kwa uwazi.
8. Amua kusuka au kunyoa
Likishatokea hilo jaribu kuzungumza na moyo wako. Uamuzi wa kuendelea kuwa naye au kumuacha uuchukue bila shinikizo. Hata kama kakuumiza, kama unadhani unaweza kumpa nafasi nyingine mpe ili usije ukajuta baadaye kwa kumkosa lakini kama unaona moyo wako unamkataa, muache.
9. Msamehe
Kwa uamuzi wowote utakaochukua ni lazima uwe tayari kumsamehe ili kuliondoa dukuduku lako rohoni. Kutokumsamehe kunaweza kukufanya ukawa unaumia kila wakati na kukosa amani.
10. Iwe fundisho kwako
Chukulia tukio hilo kama fundisho kwako. Huenda wewe ndiye uliyechangia kusalitiwa, kama ni hivyo badilika ili yasije yakakukuta kama hayo utakapokuwa na mwingine. Pia kama kusalitiwa kumetokana na kutoridhika kwa mpenzi wako, kuwa makini wakati wa kuchagua mwingine wa kuwa naye.
Lakini licha ya kwamba usaliti si kitu kizuri, watu wamekuwa wakisalitiana, tena sana tu. Inafika wakati unashindwa kuamini kama yupo mtu ambaye hajawahi kumsaliti mpenzi wake.
Niseme tu kwamba wapo wachache waliotulia ila asilimia kubwa ya walio kwenye uhusiano ni wasaliti hata tafiti zimethibitisha hilo. Kama hali yenyewe iko hivyo, cha kujiuliza ni kwamba unapobaini mpenzi wako kakusaliti ni kipi unachotakiwa kufanya? Je, ni kuamua kunywa sumu kama ambavyo wamekuwa wakifanya wengine? Sidhani kama huo ni uamuzi sahihi.
Mtaalam wa masuala ya mapenzi James Johnson kutoka Marekani amependekeza mambo 10 unayoweza kufanya baada ya kubaini kuwa mpenzi wako amekusaliti.
1. Kubaliana na kilichotokea
Kama kishakusaliti ni tukio ambao limeshatokea na haliwezi kufutika. Kubali kuwa umetendwa, huzunika lakini mwisho liache lipite ili uweze kujipanga upya.
2. Usijilaumu
Wapo ambao wakishasalitiwa hujuta kukubali kuingia kwenye uhusiano na watu waliowatenda. Utamsikia mtu akisema ‘najuta kumkubalia awe mpenzi wangu’. Kujilaumu kwa namna hiyo hukutakiwi kwani kutakufanya uzidi kunyong’onyea.
3. Jitoe
Jifanye kama vile aliyesalitiwa siyo wewe bali ni rafiki yako kisha jiulize ungemshaurije? Ushauri ambao ungempata basi uchukue kisha uufanyie kazi.
4. Pima ulivyoathirika
Je, kitendo cha mpenzi wako kukusaliti kimekukosesha imani juu yake? Kama ni hivyo, unadhani una sababu ya kuendelea kuwa naye au unahisi madhara aliyokupatia huwezi kumvumilia?
5. Mpasulie ukweli
Kwa vyovyote utakavyoamua ni lazima umweleze juu namna alivyokuumiza kwa usaliti wake. Hata kama utampa nafasi nyingine lazima ajue jinsi alivyokuumiza ili iwe changamoto kwake.
6. Chunguza kwa nini kakusaliti
Usiliache likapita hivi hivi, unatakiwa kujua sababu ya yeye kukusaliti. Je, kuna ambacho anakikosa kwako au ni tamaa zake tu? Jibu utakalolipata litakusaidia katika maisha yako ya kimapenzi.
7. Usikubali akulainishe
Huenda huyo mpenzi wako ni ‘msanii’ na anaweza kukulainisha kwa maneno ambayo yanaweza kukufanya ukalichukulia tukio hilo kiurahisi. Kuwa na msimamo na eleza hisia zako kwa uwazi.
8. Amua kusuka au kunyoa
Likishatokea hilo jaribu kuzungumza na moyo wako. Uamuzi wa kuendelea kuwa naye au kumuacha uuchukue bila shinikizo. Hata kama kakuumiza, kama unadhani unaweza kumpa nafasi nyingine mpe ili usije ukajuta baadaye kwa kumkosa lakini kama unaona moyo wako unamkataa, muache.
9. Msamehe
Kwa uamuzi wowote utakaochukua ni lazima uwe tayari kumsamehe ili kuliondoa dukuduku lako rohoni. Kutokumsamehe kunaweza kukufanya ukawa unaumia kila wakati na kukosa amani.
10. Iwe fundisho kwako
Chukulia tukio hilo kama fundisho kwako. Huenda wewe ndiye uliyechangia kusalitiwa, kama ni hivyo badilika ili yasije yakakukuta kama hayo utakapokuwa na mwingine. Pia kama kusalitiwa kumetokana na kutoridhika kwa mpenzi wako, kuwa makini wakati wa kuchagua mwingine wa kuwa naye.
AFIA MAHAKAMANI AKISUBIRI KUMWEKEA DHAMANA MTOTO WAKE....
MTU mmoja aliyefahamika kwa
jina la Tiger Mwaigomole (70) Mkazi wa kata ya Masukulu wilayani Rungwe
amefariki dunia ghafla akiwa katika chumba cha Mahakama ya Wilaya ya
Rungwe akifuatilia mwenendo wa kesi inayomkabili mtoto wake wakati
Mahakama ikiendelea.
Tukio hilo la aina yake lilitokea hivi karibuni majira ya saa 9 alasiri ndani ya Mahakama hiyo ambapo Marehemu alifika mahakamani hapo akiwa na mwanaye aliyejulikana kwa jina la Lusajo Tiger (40) wakiwa na lengo la kumwekea dhamana ndugu yao Gwakisa Tiger ambaye alifikishwa mahakamani hapo akituhumiwa kwa kosa la kupigana na kujeruhi katika ugomvi uliotokea kijijini kwao.
Kwa mujibu wa mtoto wa Marehemu aliyekuwa ameongozana nae Mahakamani hapo Lusajo Tiger alisema wakati kesi ikiendelea chini ya Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Rungwe, Kingwele, ndugu yao alipandishwa kizimbani kusomewa mashtaka yanayomkabili ndipo marehemu alipoanza kutetemeka kwa madai kuwa anajisikia baridi kali sana.
Alisema kutokana na marehemu kulalamikia baridi aliamua kumnunulia chai ya moto ili anywe na kupunguza baridi ambapo baada ya kufanya hivyo marehemu alikata roho muda mfupi baada ya kumaliza kunywa chai aliyokuwa amepelekewa huku akiwa amekaa ndani ya chumba cha mahakama hiyo.
Kutokana na tukio hilo Askari polisi waliokuwepo mahakamani hapo waliuchukua mwili wa marehemu na kuukimbiza katika Hospitali ya Wilaya ya Rungwe Makandana kwa ajili ya vipimo lakini hata hivyo mwili ulikabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya taratibu za mazishi ingawa ripoti ya kifo chake haikutolewa mapema.
Wakati huo huo Hukumu ya kesi ya mauaji dhidi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Rungwe, John Mwankenja inayowakabili Hakimu Mwakalinga na wenzie watatu huenda ikatolewa Novemba 11 mwaka huu baada ya Mahakama kuu kanda ya Mbeya chini ya Jaji Samwel Karua kumaliza kusikiliza ushahidi wa upande wa mashtaka pamoja na utetezi kwa upande wa watuhumiwa.
Kwa mujibu wa Jaji Karua alisema baada ya kumaliza kusikiliza pande zote mbili atatumia muda wa siku mbili kwa ajili ya kuandika hukumu ambayo itaitoa Novemba 11, Mwaka huu, kesi ambayo inasimamiwa na Mwanasheria wa Serikali Archiles Mulisa huku watuhumiwa wakitetewa na Mawakili wawili wa kujitegemea ambao ni Simon Mwakolo na Victor Mkumbe.
Tukio hilo la aina yake lilitokea hivi karibuni majira ya saa 9 alasiri ndani ya Mahakama hiyo ambapo Marehemu alifika mahakamani hapo akiwa na mwanaye aliyejulikana kwa jina la Lusajo Tiger (40) wakiwa na lengo la kumwekea dhamana ndugu yao Gwakisa Tiger ambaye alifikishwa mahakamani hapo akituhumiwa kwa kosa la kupigana na kujeruhi katika ugomvi uliotokea kijijini kwao.
Kwa mujibu wa mtoto wa Marehemu aliyekuwa ameongozana nae Mahakamani hapo Lusajo Tiger alisema wakati kesi ikiendelea chini ya Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Rungwe, Kingwele, ndugu yao alipandishwa kizimbani kusomewa mashtaka yanayomkabili ndipo marehemu alipoanza kutetemeka kwa madai kuwa anajisikia baridi kali sana.
Alisema kutokana na marehemu kulalamikia baridi aliamua kumnunulia chai ya moto ili anywe na kupunguza baridi ambapo baada ya kufanya hivyo marehemu alikata roho muda mfupi baada ya kumaliza kunywa chai aliyokuwa amepelekewa huku akiwa amekaa ndani ya chumba cha mahakama hiyo.
Kutokana na tukio hilo Askari polisi waliokuwepo mahakamani hapo waliuchukua mwili wa marehemu na kuukimbiza katika Hospitali ya Wilaya ya Rungwe Makandana kwa ajili ya vipimo lakini hata hivyo mwili ulikabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya taratibu za mazishi ingawa ripoti ya kifo chake haikutolewa mapema.
Wakati huo huo Hukumu ya kesi ya mauaji dhidi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Rungwe, John Mwankenja inayowakabili Hakimu Mwakalinga na wenzie watatu huenda ikatolewa Novemba 11 mwaka huu baada ya Mahakama kuu kanda ya Mbeya chini ya Jaji Samwel Karua kumaliza kusikiliza ushahidi wa upande wa mashtaka pamoja na utetezi kwa upande wa watuhumiwa.
Kwa mujibu wa Jaji Karua alisema baada ya kumaliza kusikiliza pande zote mbili atatumia muda wa siku mbili kwa ajili ya kuandika hukumu ambayo itaitoa Novemba 11, Mwaka huu, kesi ambayo inasimamiwa na Mwanasheria wa Serikali Archiles Mulisa huku watuhumiwa wakitetewa na Mawakili wawili wa kujitegemea ambao ni Simon Mwakolo na Victor Mkumbe.
Na Mbeya yetu
LAANA...!! PICHA ZA UCHI ZA MSANII NYOTA WA BONGO MOVIE AKICHEZEWA NYETI ZAKE NA WANAWAKE ZANASWA...

Mmh wimbo la mastaa wetu kuendelea kujishushi hadhi linaendelea kushika kasi kila kukicha huku hakuna sheria zozote zinazochukuliwa dhidi yao.
Msanii nyota toka kiwanda cha bongo movie Edward Tem "Nick" picha zake za utupu zaidi 200 zimenaswa na mtandao huu hatari zikimuonesha akiwa na wanawake zaidi ya watano amabao wanasadikika kuwa machangudoa wakimchezea nyeti zake.
Hapa tumeziweka baadhi ya picha tu ili tupate kujifunza kupitia vitendo viovu wanavyovifanya wasanii wetu hapa nchini ambao ni kioo cha jamii...
Wiki kadhaa za nyuma iliwahi kushushiwa picha za fumanizi la msanii huyo dhidi ya msanii wake wa kike ambae alifumaniwa nae maeneo ya Kawe Jijini Dar ambapo sakata hili liliishia kituo cha Polisi Hananasifu baada ya msanii huyo kuridhia kumlipa mwenye mke kiasi cha shilingi laki tano.
Chanzo chetu kiliendelea kusema kuwa picha hizi za utupu zilipigwa siku nyingi kabla ya hilo fumanizi na zimevuja kutoka kwenye kamera yake mara baada ya kupotea ambapo blog hii ilifanya jitahada za kumtafuta msanii huyo kupitia simu yake ya kiganjani lakini kwa bahati mbaya hakuweza kupatikana.
Msanii huyo ambae sasa hivi ameachia filamu zake kama Bad Father,The,re ma sons, House Girl na Boss ambapo kati ya filamu hizo moja tu ndiyo iliyopelekwa kampuni ya Pilipili Entertainment ya Bad Father...
Bofya hapo chini kuziona picha hizo za uchi za msanii huyo chipukizi wa bongo movie....
WEMA SEPETU ASEMA..! "SITASAHAU KAMWE JINA ALILOKUWA AKINIITA BABA...."
![]() |
Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ |
WEMA Isaac Sepetu ‘Madam’ amefunguka kuwa kamwe hatasahau jina la Miss World ambalo marehemu baba yake, mzee Isaac Abraham Sepetu alikuwa akimuita.
Akizungumza na mwanahabari wetu wakati wa kuaga mwili wa baba yake nyumbani kwao, Sinza-Mori jijini Dar, Jumanne iliyopita, Wema alisema baba yake alikuwa akimuita jina hilo kama utani kutokana na masuala ya urembo aliyokuwa akiyafanya hivyo alipofariki dunia jina hilo ndiyo kumbukumbu yake ya muhimu.
![]() |
Marehemu Isaac Abraham Sepetu. |
Mwili wa baba Wema ulisafirishwa Jumatano (jana) kuelekea visiwani Zanzibar kwa ajili ya mazishi.
MAMA RWAKATARE ATENGWA NA MAKANISA KWASABABU YA ILE NDOA ALIYOFUNGISHA YA MBUNGE WA CCM ALIYEOLEWA NA KIJANA MDOGO...
MBUNGE
wa Viti Maalumu, Mchungaji Getrude Rwakatare (CCM) wa Kanisa la Tanzania
Assemblies of God (TAG), Mikocheni B, jijini Dar es Salaam, ametengwa
katika Ushirikiano wa Makanisa baada ya kanisa lake kulalamikiwa
kufungisha ndoa inayodaiwa kukiuka taratibu za kikanisa, kisheria na
kimaadili, Tanzania Daima Jumatano limejulishwa.Ndoa
inayolalamikiwa
kufungishwa na kanisa hilo ni ile iliyoibuliwa na gazeti hili wiki
iliyopita ambayo inamhusisha Mbunge wa Viti Maalumu, Rosweeter Kasikila
(CCM) mwenye umri wa miaka 60 na kijana Michael Christian wa miaka 26.

Ndoa hiyo ambayo ilifungwa katika kanisa hilo Septemba Mosi mwaka 2011, imebaki kuwa gumzo na kuwaacha hoi baadhi ya mawaziri, wabunge pamoja na majirani wanaoishi jirani na mbunge huyo mjini Bagamoyo, Pwani.
Akizungumza na gazeti hili jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili na Haki za Jamii ya makanisa hayo, Mchungaji William Mwamalanga, alisema uamuzi wa kulitenga kanisa la Mama Rwakatare umetokana na kikao cha Kamati ya Maadili iliyokutana jana jijiji Dar es Salaam.
Alisema Kanisa la Mchungaji Rwakatare halifai kuendelea kuwa katika ushirika huo kutokana na kubariki ndoa hiyo aliyodai kuwa ni batili.
Mchungaji Mwamalanga alisema utaratibu wa ndoa katika makanisa unafahamika, ikiwa ni pamoja na wafungaji wa ndoa kutakiwa kutangaza ndoa hiyo hadharani kwa kipindi cha wiki tatu.
“Ndoa hii haikutangazwa hadharani, kibaya zaidi inasemekana imefungwa ndani ya ofisi na sio kanisani. Hiyo haiwezi kuitwaa ndoa maana haijakidhi vigezo na taratibu za kikanisa, ni lazima Mchungaji Rwakatare awajibike,” alisema.
Alisema lazima nyumba za ibada zikubali kutogeuzwa kichaka cha kusaidia uovu kama ilivyofanywa na kanisa hilo la Mikocheni B kwa kukubali kufanikisha ndoa hiyo kinyume cha taratibu.
“Tunalaani ndoa hiyo kuanzia mawio hadi machweo kwa kuwa hata maandiko ya kitabu kitakatifu cha Biblia kinawathamini yatima kama alivyo huyo kijana Michael anayeonekana kutoafiki ndoa hiyo kwa matakwa yake,” alisema mchungaji huyo.
Alisisitiza kuwa wanamtenga Mchungaji Rwakatare na kanisa lake kwani amewachafua na kuyatia aibu makanisa mengine yote nchini.
Mchungaji huyo pia alimtaka Mwenyekiti wa CCM taifa, Rais Jakaya Kikwete kuwaengua kwenye chama hicho Mchungaji Rwakatare na Kasikila kuhusiana na ndoa hiyo.
“Rwakatare ni mtunga sheria, anajua wazi kuwa ndoa inatakiwa pia kubandikwa katika ubao wa matangazo. Ni wazi kuwa wameamua kuvunja sheria na kutenda kosa la jinai,” alidai.
Mwamalanga alisema kuwa kwa hatua hiyo ndoa hiyo ni batili na haramu kwa kuwa ni aibu pia kwa mtoto kumuoa mwanamke mwenye umri wa mama yake.
Katika hatua nyingine, mchungaji huyo alisema umoja wao unafanya kila iwezalo kuhakikisha kijana Michael anarudishiwa vyeti vyake ambavyo kwa sasa vimezuiliwa na Mbunge Kasikila.
Pia aliitaka Kamati ya Maadili ya Bunge kuwaita na kuwahoji wabunge hao kwa kitendo chao cha kuhalalisha ndoa hiyo kwani kimeutia doa muhimili huo.
Alisema Bunge ni sehemu tukufu, hivyo Rwakatare na Kasikila hawana hadhi ya kukaa huko, hivyo alishauri waenguliwe.
Alipopigiwa simu kueleza msimamo wake juu ya uamuzi wa umoja wa makanisa hayo kumtenga kwa kuhalalisha ndoa hiyo, Mchungaji Rwakatare aling’aka na kukata simu.
Alipopigiwa tena simu yake ilizimwa na hakuweza kupatikana tena hadi tunaenda mitamboni.

Ndoa hiyo ambayo ilifungwa katika kanisa hilo Septemba Mosi mwaka 2011, imebaki kuwa gumzo na kuwaacha hoi baadhi ya mawaziri, wabunge pamoja na majirani wanaoishi jirani na mbunge huyo mjini Bagamoyo, Pwani.
Akizungumza na gazeti hili jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili na Haki za Jamii ya makanisa hayo, Mchungaji William Mwamalanga, alisema uamuzi wa kulitenga kanisa la Mama Rwakatare umetokana na kikao cha Kamati ya Maadili iliyokutana jana jijiji Dar es Salaam.
Alisema Kanisa la Mchungaji Rwakatare halifai kuendelea kuwa katika ushirika huo kutokana na kubariki ndoa hiyo aliyodai kuwa ni batili.
Mchungaji Mwamalanga alisema utaratibu wa ndoa katika makanisa unafahamika, ikiwa ni pamoja na wafungaji wa ndoa kutakiwa kutangaza ndoa hiyo hadharani kwa kipindi cha wiki tatu.
“Ndoa hii haikutangazwa hadharani, kibaya zaidi inasemekana imefungwa ndani ya ofisi na sio kanisani. Hiyo haiwezi kuitwaa ndoa maana haijakidhi vigezo na taratibu za kikanisa, ni lazima Mchungaji Rwakatare awajibike,” alisema.
Alisema lazima nyumba za ibada zikubali kutogeuzwa kichaka cha kusaidia uovu kama ilivyofanywa na kanisa hilo la Mikocheni B kwa kukubali kufanikisha ndoa hiyo kinyume cha taratibu.
“Tunalaani ndoa hiyo kuanzia mawio hadi machweo kwa kuwa hata maandiko ya kitabu kitakatifu cha Biblia kinawathamini yatima kama alivyo huyo kijana Michael anayeonekana kutoafiki ndoa hiyo kwa matakwa yake,” alisema mchungaji huyo.
Alisisitiza kuwa wanamtenga Mchungaji Rwakatare na kanisa lake kwani amewachafua na kuyatia aibu makanisa mengine yote nchini.
Mchungaji huyo pia alimtaka Mwenyekiti wa CCM taifa, Rais Jakaya Kikwete kuwaengua kwenye chama hicho Mchungaji Rwakatare na Kasikila kuhusiana na ndoa hiyo.
“Rwakatare ni mtunga sheria, anajua wazi kuwa ndoa inatakiwa pia kubandikwa katika ubao wa matangazo. Ni wazi kuwa wameamua kuvunja sheria na kutenda kosa la jinai,” alidai.
Mwamalanga alisema kuwa kwa hatua hiyo ndoa hiyo ni batili na haramu kwa kuwa ni aibu pia kwa mtoto kumuoa mwanamke mwenye umri wa mama yake.
Katika hatua nyingine, mchungaji huyo alisema umoja wao unafanya kila iwezalo kuhakikisha kijana Michael anarudishiwa vyeti vyake ambavyo kwa sasa vimezuiliwa na Mbunge Kasikila.
Pia aliitaka Kamati ya Maadili ya Bunge kuwaita na kuwahoji wabunge hao kwa kitendo chao cha kuhalalisha ndoa hiyo kwani kimeutia doa muhimili huo.
Alisema Bunge ni sehemu tukufu, hivyo Rwakatare na Kasikila hawana hadhi ya kukaa huko, hivyo alishauri waenguliwe.
Alipopigiwa simu kueleza msimamo wake juu ya uamuzi wa umoja wa makanisa hayo kumtenga kwa kuhalalisha ndoa hiyo, Mchungaji Rwakatare aling’aka na kukata simu.
Alipopigiwa tena simu yake ilizimwa na hakuweza kupatikana tena hadi tunaenda mitamboni.
- Tanzania Daima
HATIMAYE UVUMILIVU WAMSHINDA IRENE UWOYA NA KUANZA KUSHUSHA MATUSI MTANDAONI ...KISA BOFYA HAPA
“...Wale ma-(Tusi linalohusisha kiungo cha mwili) wanao post (Tusi kama la hapo mwanzo) humu...waaandike watakavyo...sio (Tusi- vitendo vibaya kwenye jamii) tuuu yan na vza yakuzunguka dunia nzima....siitaj watu ma-(Tusi kali sana)...kama
na kuboa kafe mbele....eti range nimehongwa mtasubiri sanaaaa....sina
mdaa huo sinaaa...wakukaa pemben na kumsmanga mtuuuu...wote mnao ni
disss ma-(Tusi la kumalizia sentensi)...”
Hayo ni maneno ya mwadada Irene Uwoya aliyoaandika usiku wa leo hii
kupitia ukurasa wake wa mtandao mmoja wa kijamii. Tulipoyasoma tuu,
tulishtushwa sana kwani si kawaida kwa mwanadada huyu kuandika maneno
mzito kama haya na ndipo tulipoamua kufanya utafiti yakinifu ili tujue
why??? Na haya ndo majibu ya uchunguzi wetu huu…

Tujikumbushe Historia fupi
Hivi majuzi mwadada Irene Uwoya alipost kwenye mtandao picha za
gari yake mpya aina ya Range Rover na ndipo watu wengi walianza
ku-comment na “kumponda” mwanadada huyu kuwa sio yake bali kahongwa na
wanaume “wanaomuweka mjini”
Irene akajibu
Siku
si nyingi baadae Irene aliwajibu kwa kusema kuwa gari hiyo ni yake na
wote wanaosema kahongwa watasubiri sana maana hiyo ni matokeo ya jasho
lake
Msiba wa baba yake wema wahusishwa
Kwa bahati mbaya mwanadada Wema Sepetu alipata matatizo ya kufiwa na baba yakehivi
majuzi na ndipo zikatoka tetesi kuwa ETI mwanadada Irene pamoja na
kundi jingine la mastaa Fulani wamesusa kuhudhuria msiba huo kwa madai
kuwa Wema huwa hashiriki misiba ya wengine
Mashabiki wa wema wamjia juu
Baada ya mambo hayo yote hapo juu ndipo kundi la mashabiki wa wema
walipoanza kuandika kwenye ukurasa wa mwanadada huyo, wakimutukana na
kumponda sana eti hilo gari sio lake bali kahongwa na jamaa mmoja hivi
(Jina tunalihifadhi kwa sababu za kiusalama) na hivyo asiwadanganye
wananchi mambo ambayo si kweli
Uvumilivu ukawa mchache kwa Irene
Baada ya matusi na maneno mengi ya kejeli toka kwa mashabiki hao
kumzidi Irene hatimaye ndio ameamua kuandika hayo hapo unayoyaona juu.
Daah, hatari sana mjini hapa ukiwa staa.
Tanzania yamzuia Benard Membe kuhudhuria vikao vya jumuiya ya Afrika Mashariki....Waziri Siita atoa wiki mbili za kuitema jumuiya hiyo
SERIKALI iko katika mazungumzo na nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Burundi ili kushirikiana kwa baadhi ya maeneo, hasa kutokana na ukweli kuwa baadhi ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Rwanda, Kenya na Uganda, zimeonesha mwelekeo wa kujitenga.
Waziri
wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, alisema hayo jana
alipokuwa akitii mwito wa Spika, Anne Makinda, kujibu maswali ya
wabunge, waliokuwa wakihoji kwa nini Tanzania nayo isijitenge.
“Kiuchumi
sisi ni majirani zaidi na DRC… Rwanda inaangalia barabara
tunayoshirikiana kuijenga kufika Burundi, ila ujenzi wa reli ya
Uvinza-Msongati itaokoa wenzetu wa Burundi, kwani wakitumia bandari ya
Mombasa kwenda Bujumbura, kwao ni mbali kwa zaidi ya kilometa 900,
tofauti na Dar es Salaam kwenda Bujumbura,” alifafanua Sitta.
Kabla
ya kutoa ufafanuzi huo, wabunge walitaka Serikali isikubali kuchezewa
na baadhi ya nchi za EAC na kuitaka ijitoe mara moja na ikiwezekana,
iunde Jumuiya yake ikishirikisha Burundi na DRC.
Aliyeibua
suala hilo la kutaka Tanzania ijitenge ni Mbunge wa Viti Maalumu, Rukia
Ahmed (CUF), ambaye katika swali lake la nyongeza aliitaka Serikali
ieleze inasubiri nini kujitoa katika Jumuiya hiyo kutokana na kuendelea
kutengwa na marais wa Rwanda, Kenya na Uganda ambao wamekuwa wakikutana
bila Tanzania na wanajumuiya wengine kushirikishwa.
Pia,
alitaka nchi ijitoe kwa kutumia Ibara ya 145 ya Mkataba wa Uanzishwaji
wa Jumuiya hiyo na kunukuu kauli ya Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe kuwa Tanzania inasubiri talaka
kutoka jumuiya hiyo.
Mbali
na swali hilo la nyongeza, katika swali la msingi, Mbunge wa Mbinga
Magharibi, John Komba (CCM), alisema kabla ya Rwanda na Burundi kujiunga
na EAC, hali ilikuwa tulivu na yenye maelewano makubwa.
Aliongeza
kuwa baada ya nchi hizo kujiunga na Jumuiya, sasa hali ni tete na
kuhoji ni kitu gani kilisababisha nchi hizo kujiunga na Jumuiya na kwa
nini Tanzania isijitoe kama ilivyofanya kwenye Soko la Pamoja la Nchi za
Mashariki na Kusini mwa Afrika (COMESA).
Mbunge
wa Same Mashariki, Anne Kilango-Malecela (CCM), alitaka Tanzania
isitishe kushiriki shughuli zote za Jumuiya kwa kile alichosema
inaelekea kufa. Kutokana na uzito wa suala hilo, Spika wa Bunge, Makinda
alimtaka Waziri Sitta, kujibu maswali hayo kwa pamoja. Kero, kususa
Sitta alisema ni kweli inakera kuona wanajumuiya wengine wanaizunguka
Tanzania na kusema hawajakaa kimya katika kushughulikia suala hilo.
Alisema
kwa sasa mambo yote yanayohusu Jumuiya, ambayo baadhi ya nchi wanachama
wamekutana kwa siri na kuyatolea msimamo na kuja nayo katika mikutano
ya pamoja, Tanzania haitashiriki. Alitoa mfano wa mambo yanayohusu sera
za mambo ya nje, ambapo alisema yeye hatashiriki vikao vyote, ambavyo
wanajumuiya wengine tayari wana msimamo.
“Kesho
(leo), Burundi kuna mkutano, nimemwambia Naibu Waziri asihudhurie,
Katibu Mkuu wa Wizara atakwenda lakini hatatoa msimamo wowote wa
Serikali, maana si kazi yake, bali yetu sisi wanasiasa,” alisema Sitta.
“Tulishamhoji
Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa EAC kuhusu hili, kama tutaendelea
na uongo wa kitoto tutakuja bungeni, kwenu waheshimiwa wabunge na
kumaliza hili, hatutakubali liendelee, lakini kwa sasa tufuatilie mpaka
mwongo aumbuke,” alisema Sitta.
Alisisitiza
kwamba huu ni wakati wa kufuata ushauri wa Rais wa Awamu ya Pili, Ali
Hassan Mwinyi, aliyepata kusema “Mtu mwongo mwongoze”, na kuongeza kuwa
kama wana Jumuiya wengine wana hila, itajulikana tu, kwa kuwa hata juzi
walikutana Kigali, Rwanda bila kushirikisha Tanzania. Sitta alisema
baada ya wiki mbili, majibu ya Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa
Jumuiya hiyo, yatatolewa na hapo nchi itatoa uamuzi.
Akijibu
swali la nyongeza la Komba, aliyetaka kujua kwa nini Jumuiya hailaani
vitendo vya kuunda Jumuiya mpya ndani ya nyingine na kuitaka Tanzania
iunde Jumuiya yake na DRC na Burundi, na swali la Ahmed aliyetaka
Tanzania isisubiri talaka kujitoa, Sitta alisema haijaanzishwa Jumuiya
nyingine, ila wapo katika harakati fulani.
Kuhusu
kutosubiri talaka, Sitta alisema asilimia 52 ya eneo la Afrika
Mashariki, linaundwa na Tanzania huku asilimia 48 ikichukuliwa na nchi
nyingine, hivyo suala la nani anatoa talaka, lina uzito kwetu zaidi na
kuongeza kuwa, kama ni nani mwoaji, Tanzania ndiyo imeoa na labda ndiyo
itoe takala na si kupewa.
Msimamo
Sitta akijibu swali la Msingi la Ahmed, aliyetaka kujua msimamo wa
Serikali wa mambo yanayohusu Jumuiya hasa kutokana na mkutano
uliofanyika Mombasa siku ya ufunguzi wa bandari hiyo, kujadili pamoja na
mambo mengine, masuala ya biashara, miundombinu na Shirikisho la Afrika
Mashakiri, alisema mikutano ya wakuu wa Kenya, Rwanda na Uganda bila
kuishirikisha Tanzania, ilianza Entebbe, Uganda Juni 24 na 25.
Alisema
mkutano wa pili ulifanyika Mombasa Agosti 28 kwa kigezo cha uzinduzi
rasmi wa gati namba 19, ambayo imepangwa mahususi kushughulikia mizigo
ya Rwanda na Uganda.
"Pamoja
na suala hilo la bandari ya Mombasa, ilijitokeza kwamba wakuu hao wa
nchi tatu walijadili pia masuala ya uanzishwaji wa Himaya Moja ya
Forodha, uanzishwaji wa hati moja ya kuishi katika nchi hizo (viza) kwa
watalii, matumizi ya vitambulisho vya Taifa kwa nchi zao na harakati za
Shirikisho la Kisiasa la nchi zao.
“Kwa
kuzingatia kuwa masuala hayo yapo katika hatua mbalimbali za
majadiliano katika Jumuiya na nchi zote tano hushiriki, Tanzania katika
mkutano wa 27 wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya uliofanyika Arusha Agosti
31, tulidai ufafanuzi," alisema Sitta.
Alisema
walimtaka Mwenyekiti wa Baraza kutoa ufafanuzi wa kina kuhusu mikutano
hiyo ya utatu inayoendeshwa sambamba na mikutano ya kawaida ya kalenda
za Jumuiya na kwamba kikao cha Baraza hilo cha kutathmini hali hiyo,
kinatarajiwa kufanyika wiki ya pili ya mwezi ujao Arusha.
Sitta
alisisitiza wakati taarifa hiyo ikisubiriwa, msimamo wa Tanzania ni
kuwa masuala yote yanayojadiliwa na kuamuliwa nje ya utaratibu wa
Jumuiya, haitayatambua kama uamuzi wa Jumuiya na utekelezaji wake
utahusu nchi husika pekee.
Kifo
kujirudia? Iwapo sintofahamu hii itaendelea kama ilivyo na hata kufikia
hatua ya Tanzania kujitoa, EAC itakuwa inasambaratika kwa mara
nyingine, baada ya kutokea hivyo mwaka 1977.
Tukio
la mwaka 1977 lilitokana na nchi tatu wanachama wakati huo, Tanzania,
Kenya na Uganda, kutofautiana kisiasa huku Tanzania na Uganda zikiwa
katika uhusiano mchungu uliosababisha vita baina yao.
Wakati
Jumuiya ya kwanza ikivunjika, nchi hizi zilikuwa zikiongozwa na Mwalimu
Julius Nyerere wa Tanzania, Mzee Jomo Kenyatta wa Kenya na Dk Milton
Obote wa Uganda, ambao wote sasa ni marehemu.
Novemba
30, 2001 Jumuiya ilifufuliwa chini ya marais Mwinyi (Tanzania), Daniel
arap Moi (Kenya) na Yoweri Museveni wa Uganda katika sherehe
zilizofanyika Arusha.
Rwanda
na Burundi zilijiunga rasmi na Jumuiya hiyo Juni 18, 2007 katika
mkutano wa marais wa EAC jijini Kampala, Uganda, na kushuhudiwa na
marais Mwai Kibaki (Kenya), Museveni, Jakaya Kikwete (Tanzania), Paul
Kagame (Rwanda) na Pierre Nkurunziza (Burundi).
Tazama video ya majibu ya waziri Sitta
Tazama video ya majibu ya waziri Sitta